Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 10:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Watakapowatesa katika muji mumoja, mukimbilie katika muji mwingine. Kweli ninawaambia: hamutamaliza kuzunguka katika miji yote ya Israeli mbele ya kurudi kwa Mwana wa Mutu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 10:23
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye mufalme Yoyakimu pamoja na waaskari shujaa wake na wakubwa wote wa serikali yake waliposikia mambo yale Uria aliyosema, mufalme alitaka kumwua. Lakini Uria alipopata habari ile, alishikwa na hofu, akatoroka na kwenda Misri.


Kwa maana Mwana wa Mutu atakuja na wamalaika akitukuzwa na Baba yake, halafu atamulipa kila mutu kufuatana na matendo yake.


Kweli ninawaambia: wamoja kati ya watu wanaokuwa hapa hawatakufa mbele hawajamwona Mwana wa Mutu akikuja katika Ufalme wake.”


Wale watu wenye elimu walipokwisha kwenda, malaika wa Bwana akamutokea Yosefu katika ndoto na kumwambia: “Amuka, utwae mutoto pamoja na mama yake na mukimbilie Misri. Mukae kule mpaka nitakapokuambia kwamba urudie, kwa maana Herode anamutafuta mutoto kusudi amwue.”


Kwa sababu hiyo, nitawatumia manabii na watu wenye hekima na walimu. Mutawaua wamoja wao, mutatundika wengine juu ya misalaba, mutawapiga wengine fimbo ndani ya nyumba zenu za kuabudia na kuwafukuza muji kwa muji.


Kweli ninawaambia: watu wa kizazi hiki watabeba lazima ya mambo hayo yote.


Kwa maana kama vile umeme unavyoangaza na kuonekana katika mbingu yote, ni vile Mwana wa Mutu atakavyoonekana siku atakapokuja.


Kisha kitambulisho cha kurudi kwa Mwana wa Mutu kitaonekana katika mbingu. Nayo mataifa yote ya dunia yatakuwa katika malalamiko, na yatamwona Mwana wa Mutu akikuja katikati ya mawingu toka mbinguni, kwa uwezo na utukufu mukubwa.


Maana kweli ninawaambia: hiki kizazi hakitapita mbele ya kutimia kwa mambo hayo yote.


Lakini kama mutumishi yule ni mutu mubaya, atajisemesha yeye mwenyewe kwamba bwana wake anakawia,


Na Yesu akaongeza kusema: “Basi mukeshe, kwa sababu hamujui siku wala saa ile.


Yesu akamujibu: “Wewe umesema. Lakini zaidi ya hiyo, ninawaambia ninyi kwamba mutamwona Mwana wa Mutu akiikaa na mamlaka karibu na Mungu Mwenye Uwezo. Mutamwona vilevile akikuja katika mbingu katikati ya mawingu!”


Yesu aliposikia kwamba Yoane ametiwa katika kifungo, akaenda zake Galilaya.


Na halafu wakati ule Mwana wa Mutu ataonekana akikuja katikati ya mawingu kwa uwezo mwingi na kwa utukufu.


Ninawaambia ninyi: hatakawia kuwapatia haki. Lakini Mwana wa Mutu atakaporudia, atakuta watu wenye kumwamini katika dunia?”


Halafu wakati ule Mwana wa Mutu ataonekana akikuja katikati ya mawingu, kwa uwezo mwingi na kwa utukufu.


Kisha mambo hayo, Yesu akatembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea katika Yudea, kwa sababu Wayuda walitaka kumwua.


Mara moja ilipokuwa usiku, wanafunzi wakawasindikiza Paulo na Sila waende Beroya. Nao walipofika kule, pale pale wakaingia katika nyumba ya kuabudia ya Wayuda.


Halafu pale pale, wandugu waamini wakamusindikiza Paulo mpaka kwenye kivuko, lakini Sila na Timoteo wakabaki Beroya.


Fujo ilipokwisha, Paulo akawakusanya wanafunzi na kuwatia moyo. Kisha akaagana nao, akasafiri kwenda Makedonia.


Naye Saulo alikuwa amekubali kwamba Stefano anastahili kuuawa. Siku ile ile kanisa lililokuwa katika Yerusalema lilianza kupata mateso makubwa. Waamini wote walisambaa katika Yudea na Samaria, isipokuwa mitume tu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ