Nao udongo muzuri walimopanda mbegu, ni mufano wa watu wanaosikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mwema na kwa uhaki. Ndio wale wanaovumulia hata wanatoa matunda mazuri.
Kwa maana katika maisha yetu, tunakuwa kila mara katika hatari ya kufa kwa ajili ya Yesu, kusudi uzima wake uonekane vilevile katika mwili wetu unaokuwa wa kufa.
Heri mutu yule anayevumilia wakati anapojaribiwa, kwa maana akiisha kushinda majaribu, atapokea ile taji ya uzima ambayo Mungu aliahidia wale wanaomupenda.
Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.
“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda, nitamupa ile mana iliyofichwa. Na nitamupa vilevile jiwe dogo jeupe, na juu yake kumeandikwa jina jipya ambalo hakuna mutu yeyote anayelijua, isipokuwa tu yule anayelipewa.
“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda nitamupa ruhusa ya kula matunda ya muti wa uzima unaokuwa katika bustani ya Mungu!
Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme.