Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 10:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Lakini watakapowapeleka kwa kuhukumiwa, musijihangaishe juu ya maneno mutakayoyasema wala juu ya namna mutakavyosema, kwa maana saa ile ile mutapewa maneno mutakayoyasema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 10:19
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, kwenda! Mimi nitaongoza kinywa chako na kukufundisha cha kusema.”


Wewe utaongea naye na kumwambia yote atakayosema. Mimi nitawasaidia na kuwafundisha mambo mutakayofanya.


Lakini Yawe akaniambia: Usiseme kwamba ungali kijana. Utakwenda kwa watu ninaokutuma kwao, na maneno yote nitakayokuamuru, utayasema.


Kisha Yawe akanyoosha mukono wake, akagusa kinywa changu, akaniambia: Nimetia maneno yangu ndani ya kinywa chako.


Vilevile mutapelekwa mbele ya wakubwa na wafalme kwa ajili yangu, kusudi mutoe ushuhuda wangu mbele yao na mbele ya watu wa mataifa mengine.


“Ni kwa sababu hii ninawaambia ninyi: musijisumbue kwa ajili ya maisha yenu, kwa ajili ya chakula au kwa ajili ya kinywaji, wala musijisumbue kwa ajili ya miili yenu kwamba mutavaa nini. Uzima ni wa lazima kuliko vyakula, nao mwili ni wa lazima kuliko nguo.


“Basi musijisumbue kwa ajili ya chakula, kwa ajili ya kinywaji au kwa ajili ya nguo.


Basi musijisumbue kwa ajili ya kesho, kwa maana kesho itajisumbukia yenyewe. Kila siku ina masumbuko yake inayoitoshelea.


“Wakati watakapowapeleka kwa kuhukumiwa katika nyumba za kuabudia, au mbele ya watawala na ya wakubwa, musijihangaishe juu ya maneno mutakayojibu au yale mutakayosema,


kwa sababu Roho Mutakatifu atawafundisha saa ile ile maneno munayopaswa kusema.”


lakini hawakuweza kumushinda kwa sababu ya hekima yake na kwa sababu ya Roho Mutakatifu aliyemwongoza kusema.


Musijisumbue juu ya neno lolote, lakini katika kila neno mutoe mahitaji yenu kwa Mungu, mukimwomba, mukimusihi na kumushukuru.


Lakini Bwana alinisaidia, akanitia nguvu nipate kuitangaza Habari Njema kwa ukamilifu kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuisikia. Nami nikaokolewa toka katika kinywa cha simba.


Kama mumoja kati yenu akikosa kuwa na hekima, aiombe kwa Mungu ambaye atamupatia. Kwa maana Mungu anawapa watu wote bila upendeleo na kwa moyo mwema.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ