12 Mutakapoingia ndani ya nyumba, muwasalimie watu wanaokuwa mule, mukisema: ‘Amani kwenu.’
Ndani ya kuta zinazokuzunguka kuwe amani, nao usalama ukuwe ndani ya nyumba zako nzuri!”
Kwa ajili ya jamaa na wandugu zangu, ee Yerusalema, ninakutakia amani!
Wakisikia au wakikataa kusikia, maana hao ni watu waasi, watatambua kwamba nabii yuko katikati yao.
“Mutakapoingia katika muji au katika kijiji, mutafute mutu anayekuwa tayari kwa kuwakaribisha, nanyi mukae kwake mpaka mutakapotoka kule.
Kama watu wa nyumba ile wakiwakaribisha, wakuwe na amani ile muliyowatakia, lakini wasipowakaribisha, amani ile iwarudilie.
Yeye ametuma ujumbe wake kwa Waisraeli, akiwahubiri Habari Njema ya amani kwa njia ya Yesu Kristo, anayekuwa Bwana wa watu wote.
Basi sisi ni wajumbe wa Kristo. Kwa njia yetu, Mungu mwenyewe anawaita ninyi; na kwa hiyo tunawasihi katika jina la Kristo, mukubali kupatanishwa na Mungu.
Ninatumaini kwamba nitakuona sasa hivi na wakati ule tutasemezana pamoja uso kwa uso.
Mutamwambia kwamba Daudi anakusalimia hivi: ‘Amani ikuwe kwako, kwa jamaa yako na yote unayokuwa nayo.