Mutafanya vile vile juu ya wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu. Mutamwacha kila muzaliwa wa kwanza na mama yake kwa siku saba na siku ya nane mutanitolea.
Ilipotimia siku ya kumutahiri mutoto, ndiyo siku ya nane tangu alipozaliwa, wakamupa jina lake Yesu. Jina hili ni lile malaika alilojulisha mbele mama yake hajabeba mimba.
Akazaa mwana, ndiye muzaliwa wake wa kwanza. Akamufunika nguo za kitoto na kumulalisha katika sanduku ya kukulishia nyama, kwa sababu walikosa nafasi ya kukaa katika nyumba ya kupangisha wageni.
Kwa maana wale Mungu aliowachagua tangu zamani, ndio aliofanya mupango juu yao tangu zamani, apate kuwafananisha na Mwana wake, kusudi Mwana wake akuwe muzaliwa wa kwanza wa wandugu wengi.