24 Na wakati Yosefu alipoamuka, akafanya sawa vile malaika wa Bwana alivyomwagiza. Akamwoa Maria.
Noa akafanya yote kama vile Mungu alivyomwamuru.
Noa akafanya yote kama vile Yawe alivyomwamuru.
Basi, Musa alitimiza kwa ukamilifu kabisa maagizo yote ya Yawe.
Akatandaza pazia juu ya hema takatifu na kuweka kifuniko cha hema juu yake, kama vile alivyoamuriwa na Yawe.
Mule, mbele ya Yawe, akawasha taa zake, kama vile alivyoamuriwa na Yawe.
na kufukiza ubani wenye harufu nzuri juu yake, kama vile alivyoamuriwa na Yawe.
Kila mara walipoingia ndani ya hema au walipokaribia ile mazabahu, walinawa, kama vile Musa alivyoamuriwa na Yawe.
“Angalia bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume, naye ataitwa Emanueli,” (maana yake “Mungu yuko pamoja nasi”).
Lakini hakulala naye mpaka alipozaa yule mutoto mwanaume. Yosefu akamwita jina lake Yesu.
Ninyi ni warafiki zangu, kama mukifanya sawa ninavyowaagiza.
Kwa rafla malaika wa Bwana akatokea na mwangaza ukajaa ndani ya chumba kile. Malaika akamutikisa Petro na kumwamusha, akimwambia: “Simama upesi!” Nayo minyororo ikaanguka toka kwenye mikono yake.
Lakini usiku malaika wa Bwana akafungua milango ya kifungo, akawaondosha mitume mule na kuwaambia: