Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 1:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Hii ndiyo habari ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Maria, mama yake, alikuwa muchumba wa Yosefu. Lakini mbele hawajakaa pamoja, akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mutakatifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 1:18
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke, kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye ataponda kichwa chako, nawe utamwuma kisigino chake.”


Nani anayeweza kutoa kitu kisafi kutoka kitu kichafu? Hakuna anayeweza.


Mutu ni nini hata aweze kuwa na moyo safi? Yule aliyezaliwa na mwanamuke atapata kuwa mwenye haki?


Haya ni majina ya babu za Yesu Kristo, wa uzao wa Daudi, wa uzao wa Abrahamu. Abrahamu alizaa Isaka, Isaka alizaa Yakobo, Yakobo alizaa Yuda na wandugu zake, Yuda alizaa Peresi na Zera kutoka muke wake Tamari, Peresi alizaa Hesironi, Hesironi alizaa Ramu, Ramu alizaa Aminadabu, Aminadabu alizaa Nasoni, Nasoni alizaa Salmoni, Salmoni alizaa Boazi kutoka muke wake Rahaba, Boazi alizaa Obedi kutoka muke wake Ruta, Obedi alizaa Yese, Yese alizaa mufalme Daudi, Daudi alizaa Solomono (mama yake ndiye yule aliyekuwa muke wa marehemu Uria), Solomono alizaa Rehoboamu, Rehoboamu alizaa Abiya, Abiya alizaa Asa, Asa alizaa Yosafati, Yosafati alizaa Yoramu, Yoramu alizaa Uzia, Uzia alizaa Yotamu, Yotamu alizaa Ahazi, Ahazi alizaa Hezekia, Hezekia alizaa Manase, Manase alizaa Amoni, Amoni alizaa Yosia, Yosia alizaa Yekonia na wandugu zake, wakati Waisraeli walipohamishwa kwenda Babeli. Nyuma ya kuhamishwa kwa Waisraeli kwenda Babeli, Yekonia alizaa Saltieli, Saltieli alizaa Zerubabeli, Zerubabeli alizaa Abihudi, Abihudi alizaa Eliakimu, Eliakimu alizaa Azoro, Azoro alizaa Zadoki, Zadoki alizaa Akimu, Akimu alizaa Elihudi, Elihudi alizaa Eleazari, Eleazari alizaa Matani, Matani alizaa Yakobo, Yakobo alizaa Yosefu, yule alikuwa mume wa Maria, mama ya Yesu, anayeitwa Kristo.


Yesu alipokuwa hajamaliza kusema na lile kundi la watu, mama yake na wandugu zake wakafika. Walisimama inje wakitaka kusemezana naye.


Wakaingia ndani ya nyumba, wakamwona mutoto pamoja na mama yake, Maria. Wakapiga magoti na kumwabudu mutoto. Kisha wakafungua mizigo yao na kumutolea zawadi ya zahabu, ubani na marasi.


“Sasa Bwana amenifanyia mema kwa kunitendea hivi; ameniondolea haya ya kutokuzaa niliyokuwa nayo mbele ya watu.”


Alienda kujiandikisha kule pamoja na muchumba wake Maria ambaye alikuwa mimba.


“Mwanaume akimukuta binti aliyechumbiwa, akilala naye,


Kwa sababu hii, wakati Kristo alipokuja katika dunia alisema: “Wewe haukutaka sadaka wala matoleo. Lakini umeniumbia mwili.


Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ