Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 9:44 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

44 Mule muna vidudu visivyokufa, na moto usiozimika.]

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 9:44
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wenye zambi katika Sayuni wanaogopa, wasiomwamini Mungu wanatetemeka na kusema: Nani anayeweza kuvumilia moto huu mukali? Nani anayeweza kuvumilia ndimi za moto usiozimika?


Kisha watakwenda kuziona maiti za wale walioniasi. Wadudu watakaowakula hawatakufa, na moto utakaowachoma hautazimika hata kidogo. Watakuwa chukizo kwa watu wote.


“Kisha mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kushoto: ‘Muondoke hapa karibu nami, ninyi muliolaaniwa! Muende katika moto usiozimika hata milele, uliotayarishwa kwa ajili ya Shetani na wamalaika wake!


Halafu hawa watakwenda kwenye nafasi watakapoazibiwa kwa milele, lakini wenye haki wataingia kwenye uzima wa milele.”


Yeye anashika lungo katika mikono yake kwa kupepeta ngano. Atakusanya ngano na kuitia katika gala yake, lakini atateketeza maganda katika moto usiozimika.”


Kama mukono wako ukikukosesha, uukate! Ni heri kwako kuingia kwenye uzima wa kweli ukiwa na mukono mumoja, kuliko kuwa na mikono miwili na kwenda katika jehenamu ndani ya moto usiozimika. [


Kama muguu wako ukikukosesha, uukate. Ni heri kwako kuingia kwenye uzima wa kweli ukiwa na muguu mumoja, kuliko kuwa na miguu miwili na kutupwa katika moto wa jehenamu. [


Mule muna vidudu visivyokufa, na moto usiozimika.


Azabu yao itakuwa kuangamizwa kwa milele, na kutengwa mbali na uso wa Bwana na mbali na utukufu wa uwezo wake,


naye vilevile atakunywa divai kali ya hasira ya Mungu iliyotengenezwa pasipo kuchangwa na maji na kumimiwa ndani ya kikombe chenye kujaa kasirani yake! Na watu kama wale, watateswa ndani ya moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto mbele ya wamalaika watakatifu na mbele ya Mwana- Kondoo.


Kisha yule Mwovu aliyewadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na lenye mawe ya kiberiti yanayowaka moto, pahali yule nyama wa ajabu na yule nabii wa uongo wanapokuwa. Nao watateswa muchana na usiku, milele na milele.


Na mutu yeyote ambaye jina lake lililokosa kuandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika ziwa la moto.


Lakini watu wenye woga, wasioamini, wenye machukizo, wauaji, wazinzi, wachawi, wanaoabudu sanamu na wote wanaosema uongo, fungu lao ni katika lile ziwa la moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto. Hiki ndicho kifo cha pili.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ