Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 9:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Lakini Yesu akamushika mukono, akamwinua, naye akasimama.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 9:27
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mimi ndiye Yawe, Mungu wako, ndiye ninayeshika mukono wako. Mimi ndiye ninayekuambia: Usiogope, nitakusaidia.


Na watu wale walipokwisha kufukuzwa, Yesu akaingia ndani ya chumba, akashika mukono wa yule binti, naye akasimama.


Basi Yesu akajongea karibu naye, akamushika mukono na kumusimamisha. Naye akapona homa na kuanza kuwashugulikia.


Yesu akamusikilia huruma, akanyoosha mukono, akamugusa na kumwambia: “Ninataka utakaswe!”


Akashika mukono wa mutoto, akamwambia: “Talita kumu,” maana yake: “Kijana binti, ninakuambia, amuka!”


Yesu akashika mukono wa yule kipofu na kumupeleka inje ya kijiji. Yesu alipokwisha kupakaa mate kwa macho ya mutu yule na kuweka mikono juu yake, akamwuliza: “Unaona kitu?”


Yule pepo akalalamika, akamutikisatikisa mutoto kwa nguvu na kutoka ndani yake. Mutoto akaonekana sawa amekufa, hata watu wengi wakaanza kusema kwamba amekufa.


Yesu alipokwisha kuingia ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamwuliza hivi wakiwa peke yao: “Sababu gani sisi hatukuweza kumufukuza yule pepo?”


Jemadari akamushika yule kijana mukono akaenda naye pembeni na kumwuliza: “Uko na habari gani ya kuniambia?”


Halafu Petro akamushika mukono wa kuume na kumusimamisha. Na pale pale miguu na vifundo vya miguu yake vikakaza kwa nguvu;


Petro akamushika mukono na kumusimamisha wima. Kisha akawaita wanafunzi na wajane, akamupeleka mbele yao akiwa muzima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ