Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 9:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Mara moja baba ya mutoto akasema kwa nguvu: “Ninaamini! Lakini unisaidie kwa ajili ya kukosa kuamini!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 9:24
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Labda Yawe ataangalia mateso yangu, naye atanilipa wema kwa laana hii ninayopata leo.”


“Rudi umwambie Hezekia, mukubwa wa watu wa Yawe, na kumwambia: Mimi, Yawe, Mungu wa babu yako Daudi, nimesikia ombi lako na nimeona machozi yako. Nitakuponyesha na nyuma ya siku tatu utaenda katika nyumba ya Yawe.


Wanaopanda kwa machozi, watavuna kwa shangwe.


Unapomwazibu mutu zambi zake kwa kumwadibisha, unaharibu kama nondo kile anachokipenda. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!


Hivi ndivyo utakavyowaambia: Heri macho yangetoa machozi usiku na muchana, wala yasikome kutiririka, maana, watu wangu wamepata hasara kubwa, wameumizwa kidonda kikubwa sana.


Yesu akamwambia: “Kwa sababu gani unasema: ‘Kama unaweza?’ Yote yanawezekana kwa yule anayeamini.”


Wakati Yesu alipoona watu wengi wanazidi kukusanyika mbiombio, akamukaripia yule pepo na kumwambia: “Wewe pepo wa bubu na wa kiziwi, ninakuamuru utoke ndani ya mutu huyu wala usimurudilie tena!”


Mitume wakamwambia Bwana: “Utuongezee imani.”


Akakuja kuinama kwenye miguu ya Yesu, akilia. Machozi yake yakamwangika juu ya miguu ya Yesu, akaipanguza na nywele zake, akaibusu na kuipakaa marasi.


Halafu akamugeukia yule mwanamuke na kumwambia Simoni: “Unamwona mwanamuke huyu? Niliingia ndani ya nyumba yako, nawe haukunipa maji ya kunawa miguu yangu, lakini mwanamuke huyu amenawa miguu yangu na machozi yake na kuipanguza na nywele zake.


Petro akiwa akifikiri juu ya maana ya yale maono, Roho Mutakatifu akamwambia: “Kuna watu watatu hapa wanaokutafuta.


Naye akaniambia: ‘Kornelio, Mungu amesikia maombi yako na kukukumbuka kwa ajili ya misaada unayotoa kwa wamasikini.


Niliwaandikia nikiwa mwenye kusikitika sana na mwenye kufazaika kabisa na nikilia machozi mengi, si kwa kuwahuzunisha ninyi, lakini ni kusudi mupate kujua namna gani ninavyowapenda.


Kwa maana mumeokolewa kwa neema ya Mungu, kwa njia ya imani. Jambo hili halitokani na ninyi wenyewe, lakini ni zawadi ya Mungu.


Kwa maana Mungu amewapa ninyi neema ya kumutumikia Kristo, na si kwa kumwamini tu, lakini vilevile kwa kuteswa kwa ajili yake.


Kwa sababu hii tunawaombea siku zote kusudi Mungu wetu awawezeshe kustahili kuishi kufuatana na mwito wake. Tunaomba kwamba kwa uwezo wake atimize nia zenu zote njema na kukamilisha kazi yenu ya imani.


Wandugu, tunapaswa kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu. Inatufaa kufanya vile kwa maana imani yenu inaongezeka, nao upendo wenu ninyi kwa ninyi unazidi kuongezeka.


Nikikumbuka machozi yako, ninatamani sana kukuona kusudi nipate kujazwa na furaha.


Kama munavyojua, nyuma ya pale alikataliwa wakati alipotaka kupokea baraka toka kwa baba yake. Yeye hakukuwa tena na namna ya kugeuza tendo lake ijapokuwa alitafuta baraka ile kwa machozi.


Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.


Wakati Yesu alipoishi katika dunia, aliomba na kusihi kwa malalamiko makubwa pamoja na kutoa machozi kwa Mungu ambaye angeweza kumwokoa toka katika kifo. Mungu alimusikia Yesu kwa sababu yeye alimuheshimu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ