Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 8:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Basi Yesu akawaamuru watu waikae chini. Kisha akakamata ile mikate saba, akamushukuru Mungu, akaimega na kuwapa wanafunzi wake waigawanye kwa watu; nao wanafunzi wakaigawanya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 8:6
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walipokuwa wakikula, Yesu akatwaa mukate, akaubariki, kisha akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema: “Mutwae na mukule, huu ni mwili wangu.”


Naye akawauliza tena: “Na wakati nilipomega mikate saba na kulisha watu elfu ine, mulijaza vitunga ngapi na vipande vya mikate?” Wakamujibu: “Saba.”


Yesu akawauliza: “Muko na mikate ngapi?” Nao wakamujibu: “Tuko na mikate saba.”


Walikuwa vilevile na samaki ndogo chache. Yesu akamushukuru Mungu na kuwaambia wanafunzi wazigawanye vilevile.


Heri watumishi wale bwana wao atakaowakuta wakikesha wakati anapofika! Kweli ninawaambia: atafunga mukaba wake vizuri na kuwakaribisha kula chakula, na kubakia pale akiwashugulikia.


Alipokuwa akiikaa kula chakula pamoja nao, akatwaa mukate na kuubariki. Kisha akaumega na kuwapatia.


Halafu mama yake akawaambia watumishi: “Mufanye kila kitu atakachowaambia.”


Na vilevile vyombo vingine vilivyotoka katika muji Tiberia vilifika karibu na pahali pale walipokula mikate, Bwana alipokuwa amekwisha kushukuru Mungu.


Mutu yeyote anayeshugulika juu ya siku fulani, anafanya hivi kwa kumutukuza Bwana. Yule anayekula kila chakula, anafanya vile kwa kumutukuza Bwana; maana anamushukuru Mungu kwa ajili ya chakula chake. Na asiyekula kila chakula anafanya hivi vilevile kwa kumutukuza Bwana na kumushukuru Mungu.


Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.


Mara moja mutakapoingia katika muji, mutamukuta mbele hajakwenda kwenye nafasi ya ibada kwenye mulima kwa kula. Maana watu hawatakula mpaka kwanza yeye abariki sadaka. Kisha wale walioalikwa watakula. Hivyo muende haraka; mutakutana naye sasa hivi.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ