Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 8:38 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

38 Kwa hiyo mutu yeyote anayesikia haya juu yangu na juu ya mafundisho yangu kati ya watu wa kizazi hiki kisichokuwa na uaminifu mbele ya Mungu na chenye zambi, Mwana wa Mutu atasikia haya juu yake vilevile. Itakuwa vile, atakapokuja pamoja na wamalaika watakatifu, akitukuzwa na Baba yake.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 8:38
44 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kutoka kiti hicho kijito cha moto kilibubujika, kikatiririka. Maelfu ya watu walimutumikia, na mamilioni walisimama mbele yake. Halafu waamuzi wakajitayarisha kwa kuhukumu, na vitabu vikafunguliwa.


Wakati wa maono haya usiku, niliona kiumbe kinachofanana na mwanadamu. Akakuja katika mawingu na kumwendea yule Muzee wa zamani sana. Akakaribishwa mbele yake.


Ninyi mutakimbia kupitia bonde lile, katikati ya milima miwili ya Yawe. Mutakimbia kama vile babu zenu walivyokimbia tetemeko la inchi wakati wa utawala wa mufalme Uzia wa Yuda. Kisha Yawe, Mungu wangu, atakuja na watakatifu wote pamoja naye.


Yesu akawajibu: “Watu wa kizazi kibaya na kinachokosa uaminifu mbele ya Mungu, wanataka kuona kitambulisho. Lakini hawataona kitambulisho isipokuwa kitambulisho cha nabii Yona.


Mwana wa Mutu atawatuma wamalaika wake, nao watakusanya toka katika Ufalme wake watu wote wanaowaangusha wengine katika zambi pamoja na wote wanaofanya maovu.


Kwa maana Mwana wa Mutu atakuja na wamalaika akitukuzwa na Baba yake, halafu atamulipa kila mutu kufuatana na matendo yake.


Kweli ninawaambia: wamoja kati ya watu wanaokuwa hapa hawatakufa mbele hawajamwona Mwana wa Mutu akikuja katika Ufalme wake.”


Watu wa kizazi kibaya na kinachokosa uaminifu mbele ya Mungu wanataka kuona kitambulisho. Lakini hawataonyeshwa kitambulisho isipokuwa kitambulisho cha nabii Yona.” Kisha Yesu akawaacha na kujiendea.


Kisha kitambulisho cha kurudi kwa Mwana wa Mutu kitaonekana katika mbingu. Nayo mataifa yote ya dunia yatakuwa katika malalamiko, na yatamwona Mwana wa Mutu akikuja katikati ya mawingu toka mbinguni, kwa uwezo na utukufu mukubwa.


“Wakati Mwana wa Mutu atakapokuja katika utukufu wake pamoja na wamalaika wote, ataikaa juu ya kiti chake cha kifalme chenye utukufu.


Yesu akamujibu: “Wewe umesema. Lakini zaidi ya hiyo, ninawaambia ninyi kwamba mutamwona Mwana wa Mutu akiikaa na mamlaka karibu na Mungu Mwenye Uwezo. Mutamwona vilevile akikuja katika mbingu katikati ya mawingu!”


Yesu akamujibu: “Mbweha wako na makao yao ndani ya matundu, nao ndege wako na chicha, lakini Mwana wa Mutu hana nafasi ya kulala.”


Na halafu wakati ule Mwana wa Mutu ataonekana akikuja katikati ya mawingu kwa uwezo mwingi na kwa utukufu.


Yesu akajibu: “Mimi Ndiye! Nanyi mutamwona Mwana wa Mutu akiikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo. Mutamwona vilevile akikuja katika mbingu katikati ya mawingu!”


Hakuna kitu chochote mutu anachoweza kutoa kwa kukomboa uzima wake.


Akawajibu: ‘Ninawaambia kwamba mutu anayekuwa na kitu ataongezewa kingine, lakini mutu asiyekuwa na kitu ataondolewa hata kidogo anachokuwa nacho.


Kwa hiyo mutu yeyote anayesikia haya juu yangu na juu ya mafundisho yangu, Mwana wa Mutu atasikia haya juu yake vilevile. Itakuwa vile atakapokuja katika utukufu wake, akitukuzwa na Baba yake pamoja na wamalaika wake watakatifu.


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Yesu akaongeza kumwambia: “Kweli, kweli, ninawaambia: mutaona mbingu zimefunguka na wamalaika wa Mungu wakipanda na kushuka mpaka kwenye Mwana wa Mutu!”


Na lile kundi la watu wakamujibu: “Sisi tumesikia katika maandiko ya Sheria kwamba Kristo ataishi milele. Basi namna gani unaweza kusema kama Mwana wa Mutu anapaswa kunyanyuliwa juu? Na huyu Mwana wa Mutu ni nani?”


Vilevile amemupa Mwana mamlaka ya kuhukumu, kwa sababu yeye ni Mwana wa Mutu.


Nao wakamujibu: “Tumetumwa hapa na Kornelio, mukubwa wa waaskari. Yeye ni mutu wa haki na mwenye kumutii Mungu, naye anasifiwa na Wayuda wote. Malaika mutakatifu amemutokea na kumwagiza akuite ufike kwake kusudi asikie maneno utakayomwambia.”


Basi mitume wakatoka katika baraza, wakifurahi sana kwa sababu walistahili kuzarauliwa kwa kuteswa kwa ajili ya Yesu.


Mimi sisikii haya juu ya Habari Njema, kwa sababu huo ndio uwezo wa Mungu unaowaokoa wote wanaoamini, kwanza Wayuda na kisha watu wa mataifa mengine vilevile.


Na mimi kwa ngambo yangu sitaki kujivuna, isipokuwa tu kwa ajili ya musalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Maana kwa njia ya musalaba huo, ninahesabu dunia kama vile imekwisha kufa na mbele ya dunia mimi ninahesabiwa kama vile mufu.


Yawe alikuja kutoka mulima Sinai, alitutokea kutoka mulima Seiri, aliangaza kutoka mulima Parani. Alitokea kati ya maelfu ya wamalaika, na moto unaowaka katika mukono wake wa kuume.


Ninyi peke yenu tu ndio tumaini, furaha, na taji ya ushindi tutakavyojivunia wakati Bwana Yesu Kristo atakaporudia.


Vilevile aitie mioyo yenu nguvu nanyi mutapata kuwa watakatifu na bila kosa mbele ya Mungu Baba yetu siku Bwana wetu Yesu atakaporudia pamoja na watakatifu wake wote.


na kwa sababu hiyo ninapata mateso haya. Lakini sisikii haya kwa ajili ya ile. Maana ninajua ni nani yule niliyemwamini, nami ninahakikisha kwamba anaweza kuchunga kile alichonipa kwa kunilinda mpaka Siku ile ya kurudi kwake.


Bwana awajalie mema sana watu wa jamaa ya Onesiforo, kwa maana amekuja mara nyingi kunifariji, wala hakusikia haya kwa kuniona niko katika kifungo.


Basi, usisikie haya ya kutoa ushuhuda kwa ajili ya Bwana wetu, wala usisikie haya kwa sababu yangu mimi ninayekuwa katika kifungo kwa ajili yake. Lakini ushiriki nami katika mateso kwa ajili ya Habari Njema, kufuatana na uwezo unaopewa na Mungu.


Lakini kwa hakika walitamani sana inchi inayokuwa bora zaidi, ndiyo inchi ya mbinguni. Kwa sababu hii Mungu hasikii haya kuitwa Mungu wao, maana amewatayarishia muji.


Aliona kwamba kupatishwa haya kwa ajili ya Kristo kuna faida kubwa zaidi kuliko kupata utajiri wote wa inchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia kupokea zawadi yake.


Basi tumwendee mbali na kambi, tukikubali kuzarauliwa kama vile yeye alivyozarauliwa.


Ninyi watu wasiokuwa na uaminifu! Hamujui kwamba kupenda raha ya dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi yeye anayetaka kupenda raha za dunia anajifanya mwenyewe kuwa adui wa Mungu.


Yule anayemukana Mwana, anamukana Baba vilevile, lakini yule anayemukubali Mwana, anamukubali Baba vilevile.


Na sasa watoto wangu, mukae ndani yake kusudi tukuwe na tumaini hakika wakati atakapotokea, na kutosikia haya mbele yake siku atakaporudi.


naye vilevile atakunywa divai kali ya hasira ya Mungu iliyotengenezwa pasipo kuchangwa na maji na kumimiwa ndani ya kikombe chenye kujaa kasirani yake! Na watu kama wale, watateswa ndani ya moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto mbele ya wamalaika watakatifu na mbele ya Mwana- Kondoo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ