Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 8:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 “Ninawasikilia watu hawa huruma, kwa sababu wamekaa nami sasa muda wa siku tatu, nao hawana chakula tena.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 8:2
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Elia alipoangalia, akaona mukate uliokaangwa juu ya makaa, na chupa ya maji karibu na kichwa chake. Basi, akakula, akakunywa na akalala tena.


Kama vile baba anavyohurumia mwana wake, ndivyo Yawe anavyohurumia wote wanaomwabudu.


Viumbe vyote vinakutazamia, nawe unavipatia chakula chao kwa wakati wake.


Yawe ni mwenye huruma na rehema; yeye hakasiriki upesi, amejaa wema.


Utatuhurumia tena; utatupilia mbali zambi zetu, utazitupa zote katika vilindi vya bahari.


Yesu alipotoka ndani ya chombo, akaona kundi kubwa la watu, naye akawasikilia huruma, akawaponyesha wale waliokuwa wagonjwa kati yao.


Yesu akawasikilia huruma. Akagusa macho yao, na mara moja wakapata kuona, nao wakamufuata.


Yesu alipoona kundi la watu, aliwasikilia huruma, kwa maana walikuwa wamesumbuka na kuregea, kama kondoo wasiokuwa na muchungaji.


Yesu akamusikilia huruma, akanyoosha mukono, akamugusa na kumwambia: “Ninataka utakaswe!”


Yesu hakumuruhusu, lakini akamwambia: “Kwenda kwako kwenye jamaa yako, na uwaelezee mambo Bwana aliyokutendea na namna alivyokuhurumia.”


Basi wakaenda peke yao ndani ya chombo kwa pahali penye ukiwa.


Wakati Yesu alipotoka ndani ya chombo, akaona kundi kubwa la watu, akawasikilia huruma, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasiokuwa na muchungaji. Basi akaanza kuwafundisha maneno mengi.


Kama nikiwaambia waende kwao pasipo kula wataregea katika njia, kwa maana wamoja kati yao wametoka mbali.”


Na mara nyingi huyu pepo anamutupa katika moto na ndani ya maji, kusudi amwue. Lakini kama unaweza kufanya kitu, utuhurumie na kutusaidia.”


Kisha akafunga safari yake na kurudia kwa baba yake. “Alipokuwa angali mbali kidogo, baba yake akamwona, akamusikilia huruma. Akamukimbilia, akamukumbatia mwana wake na kumubusu.


Bwana alipomwona yule mama, akamusikilia huruma na kumwambia: “Usilie.”


Kwa hiyo ilimupasa afanane na wandugu zake katika mambo yote, kusudi apate kuwa Kuhani Mukubwa anayekuwa mwenye huruma na mwaminifu katika kazi yake mbele ya Mungu, na kwa njia hiyo zambi za watu zisamehewe.


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


Kwa kuwa yeye mwenyewe ni muzaifu, anaweza kuwavumilia wale waliopotoka bila kujua.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ