Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 8:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Yesu akawaagiza: “Mujiangalie vizuri, mujiepushe na chachu ya Wafarisayo na ya Herode.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 8:15
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha, mufalme Daudi akamwambia Solomono mwana wake: “Uwe imara na hodari, ufanye kazi hii. Usiogope wala kuwa na wasiwasi. Yawe Mungu ambaye ni Mungu wangu, yuko pamoja nawe. Hatakuachilia lakini atakuwa nawe mpaka itakapomalizika kazi yote ambayo inayohitajika kufanyiwa kwa nyumba ya Yawe.


Mwana wangu, ukiacha kusikiliza mafundisho, mara moja utapotea mbali na maneno ya maarifa.


Sadaka yoyote ya ngano utakayomuletea Yawe inapaswa kuwa imetengenezwa bila chachu, maana hakuna ruhusa hata kidogo ya kutumia chachu wala asali katika sadaka Yawe anazotolewa kwa moto.


Katika siku zile, Herode, liwali wa jimbo la Galilaya, akasikia habari za Yesu.


Herode alikuwa amemukamata Yoane akamufunga minyororo na kumutia ndani ya kifungo. Herode alifanya vile kwa sababu ya Herodia, muke wa ndugu yake Filipo.


Na ilikuwa kwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, binti ya Herodia akacheza mbele ya wote walioalikwa. Binti yule akamupendeza Herode sana


Yesu akawaambia: “Muangalie vizuri, mujiepushe na chachu ya Wafarisayo na Wasadukayo.”


Wafarisayo wamoja na watu wamoja waliojiunga na Herode walitumwa kwa Yesu kusudi wamunase katika masemi.


Wanafunzi walikuwa wamesahau kupeleka mikate, isipokuwa walikuwa na mukate mumoja tu ndani ya chombo.


Wanafunzi wakaanza kusemezana: “Anasema hivi kwa sababu hatuna mikate.”


Kisha Yesu akawaambia watu wote: “Muangalie, mujilinde na tamaa yote ya mali, kwa sababu mali haiwezi kukinga uzima wa mutu, hata akiwa tajiri sana.”


Ninakuagiza mbele ya Mungu na mbele ya Kristo Yesu na ya wamalaika watakatifu, ushike kanuni hizo bila kuwazia mutu kitu wala kuwa na upendeleo katika mambo yote unayofanya.


Mbele ya Mungu anayevipatia vitu vyote uzima, na mbele ya Kristo Yesu aliyetoa ushuhuda wa kweli mbele ya Pontio Pilato, ninakuagiza maneno haya:


Uwakumbushe watu maneno hayo yote na kuwaonya wazi mbele ya Mungu waache kubishana juu ya maneno. Mabishano hayana faida kwa maana yanawapoteza wale wanaoyasikia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ