Yesu akaugua sana kwa huzuni, na kusema: “Sababu gani ninyi watu wa kizazi hiki munataka kuona kitambulisho? Kweli ninawaambia, hamutaonyeshwa kitambulisho!”
Halafu watu wote wa inchi ya Wagerasi wakashikwa na woga mukubwa, kwa hiyo wakamwomba Yesu aondoke kwao. Basi Yesu akaingia ndani ya chombo, kusudi apate kuondoka kule.
Basi muaminie mwangaza ule wakati mungali nao, kusudi mukuwe watu wa mwangaza.” Yesu alipokwisha kusema maneno hayo, akajiendea na kujificha mbali na lile kundi.
Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ninajiendea, nanyi mutanitafuta, lakini mutakufa katika zambi zenu. Na zaidi ya hii hamuwezi kufika pahali ninapokwenda.”
Lakini wakati Wayuda walipingana naye na kumutukana, kwa hiyo akakunguta mavumbi yaliyorukia juu ya nguo zake na kuwaambia: “Lazima ya kuazibiwa kwenu ikuwe juu ya kichwa chenu wenyewe! Mimi sina kosa. Tangu sasa nitawaendea watu wa mataifa mengine.”
Tukapanda ndani ya chombo kilichotoka Adramiti, kilichokuwa tayari kupitia kwenye vivuko vya jimbo la Azia. Halafu tukaondoka tukiwa pamoja na mwanainchi mumoja wa Makedonia aliyeitwa Aristarko, wa Tesalonika.