Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 8:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Wafarisayo wakamufikia Yesu na kuanza kubishana naye. Wakamupima wakimwomba awaonyeshe kitambulisho kinachohakikisha kwamba uwezo wake umetoka kwa Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 8:11
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo watu wakamunungunikia Musa wakisema: “Utupatie maji ya kunywa.” Musa akawauliza: “Mbona munaninungunikia? Mbona munamujaribu Yawe?”


Pahali pale Musa akapaita “Masa” na “Meriba”, ni kusema “Ujaribu” na “Magombano”, kwa sababu Waisraeli walimugombanisha na kumujaribu Yawe wakisema: “Kweli Yawe yuko pamoja nasi?”


Tunayoona sisi, ni kwamba wenye kiburi ndio wenye furaha siku zote. Watu waovu, ingawa wanastawi, hata wanapomujaribu Mungu, hawapati azabu.


Halafu walimu wamoja wa Sheria na Wafarisayo wamoja wakamwambia Yesu: “Mwalimu, tunataka kuona kitambulisho toka kwako.”


Wafarisayo wamoja wakamufikia kwa kumupima, wakamwuliza: “Sheria yetu inamuruhusu mutu kumufukuza muke wake haizuru kwa sababu gani?”


Yesu akaingia ndani ya hekalu. Alipokuwa akifundisha, wakubwa wa makuhani pamoja na wasimamizi wa watu wakamufikia na kumwuliza: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka yale?”


Wafarisayo walienda kufanya shauri kusudi wapate kumunasa Yesu katika masemi.


Lakini kwa kuwa Yesu alijua makusudi yao mabaya, akawajibu: “Ninyi wanafiki, kwa sababu gani munanipima?


Siku ile ile, Wasadukayo wamoja wakamufikia Yesu. (Watu hawa ndio wanaosema kwamba wafu hawatafufuka.)


Lakini kwa kuwa Yesu alitambua kwamba wao ni wanafiki, akawaambia: “Sababu gani munanipima? Muniletee kikoroti kimoja cha feza hapa kusudi nikione.”


Na wakati walimu wa Sheria wa kikundi cha Wafarisayo walipomwona Yesu akikula pamoja na watu wale, wakawauliza wanafunzi wake: “Kwa sababu gani anakula pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”


Yesu akawauliza wanafunzi wake: “Munabishana nao juu ya nini?”


Halafu mwalimu mumoja wa Sheria akasimama na kumwuliza Yesu kwa kumupima: “Mwalimu, nifanye nini kusudi nipate uzima wa milele?”


Na wengine walitaka kumupima wakimwomba awaonyeshe kitambulisho kinachohakikisha kwamba uwezo wake umetoka kwa Mungu.


Basi Yesu akamwambia: “Ninyi hamuwezi kuamini hata kidogo kama musipoona vitambulisho na maajabu.”


Wakamwuliza: “Basi utatuonyesha kitambulisho gani kusudi tupate kukiona na kukuamini? Utafanya jambo gani?


Ni nani kati ya wakubwa wetu au kati ya Wafarisayo aliyemwamini?


Wao walisema hivi kwa kumupima, kusudi wapate sababu ya kumushitaki. Lakini Yesu akainama na kuandika juu ya udongo kwa kidole chake.


Halafu Petro akamwambia: “Namna gani mulipatana kwa kumupima Roho wa Bwana? Sikiliza! Wale wanaotoka kumuzika mume wako wamefika hapa kwenye mulango, nao watakupeleka vilevile.”


Vilevile tusimupime Bwana kama vile wamoja wao walivyofanya, hata wakauawa na nyoka.


“Musimujaribu Yawe, Mungu wenu, kama vile mulivyomujaribu huko Masa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ