Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 7:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Munajua vizuri namna ya kutupilia amri za Mungu kusudi mushike desturi zenu!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 7:9
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ee Yawe, sasa ni wakati wa kutenda kitu, kwa maana watu wanavunja sheria yako.


Watu wameichafua dunia maana wamezivunja sheria za Mungu, wamegeuka mbali na masharti yake, wamelivunja agano lake la milele.


Bwana anasema: Watu hawa wanakuja kuniabudu kwa maneno tu, lakini mioyo yao iko mbali nami. Wananiheshimu kulingana na desturi ya watu tu, jambo walilojifunza wao wenyewe.


Mufalme atafanya kama anavyopenda. Atajitukuza na kujivuna kwamba yeye ni mukubwa kuliko miungu yote, na kumutukana Mungu wa miungu. Ataendelea kufanikiwa mpaka kasirani ifikie ukomo wake, maana yaliyopangwa sherti yatimie.


Huyo atasema maneno ya kujivuna mbele ya Mungu Mukubwa na kuwatesa watakatifu wake. Atajaribu kubadilisha sikukuu na sheria zao, na watakatifu watatiwa katika mikono yake kwa muda wa miaka mitatu na nusu.


Hivi munazarau Neno la Mungu kwa ajili ya desturi zenu munazopokezana. Nanyi munafanya mambo mengine mengi ya namna ile.”


Ilikuwa vile kwa maana Wafarisayo na Wayuda wote wanashika desturi za babu zao; zinazokataza kula pasipo kunawa mikono kama inavyostahili.


Basi Wafarisayo na walimu wa Sheria wakamwuliza Yesu: “Sababu gani wanafunzi wako hawafuati desturi za babu zetu, lakini wanakula chakula na mikono michafu?”


Basi ni kusema kwa sababu ya imani ile tunaitupilia Sheria? Hapana hata kidogo! Lakini tunasimamisha Sheria.


Hii inatokana na kuona jinsi munavyomukubali mutu yeyote anayekuja kwenu na kuwahubiri habari za Yesu mwingine asiyekuwa yule sisi tuliyemuhubiri. Na zaidi ya hii munakubali upesi kupokea roho ingine na ujumbe mwingine vinavyokuwa tofauti na Roho au Habari Njema muliyopokea toka kwetu.


Nami niliendelea vizuri sana katika dini ya Kiyuda kuwapita watu wote wengine wa kabila langu wenye umri wangu, nikijikaza sana kushika desturi za babu zetu.


Mimi sitaki kukataa neema ya Mungu kwa maana ikiwa wanaweza kuhesabiwa haki mbele ya Mungu, kwa njia ya kushika Sheria, basi Kristo alikufa bure.


Yeye atapinga kitu chochote watu wanachohesabu kuwa cha kimungu au wanachoabudu na kujiweka kuwa juu ya vyote. Yeye ataenda hata kuingia katika hekalu la Mungu na kukaa mule na kujiita mwenyewe kuwa Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ