Basi Wafarisayo na walimu wa Sheria wakamwuliza Yesu: “Sababu gani wanafunzi wako hawafuati desturi za babu zetu, lakini wanakula chakula na mikono michafu?”
Pale kulikuwa mitungi sita iliyotengenezwa kwa mawe iliyotumiwa na Wayuda kwa kutilia maji ya kujitakasa. Ndani ya kila mumoja kuliweza kuingia yapata litre mia moja za maji.
Nami niliendelea vizuri sana katika dini ya Kiyuda kuwapita watu wote wengine wa kabila langu wenye umri wangu, nikijikaza sana kushika desturi za babu zetu.
Mujiangalie hata mutu asiwapotoshe kwa elimu yake ya udanganyifu mutupu inayotegemea desturi za watu na roho mbaya zinazotawala dunia, lakini haitegemei mafundisho ya Kristo.
Kwa maana munajua namna gani mulivyokombolewa toka katika tabia za ovyo ovyo mulizoambukizwa na babu zenu. Hamukukombolewa kwa njia ya vitu vinavyoharibika kama vile feza au zahabu.