Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 7:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Mwanamuke yule akamujibu: “Bwana, unasema ukweli, lakini hata imbwa wanazoea kula makombo watoto wanayoyaangusha chini ya meza.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 7:28
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Unafumbua mukono wako kwa moyo safi, unatimiza mahitaji ya kila kiumbe kinachoishi.


Munigeukie mimi mupate kuokolewa, popote munapokuwa katika dunia. Maana mimi ni Mungu, wala hakuna mwingine.


Yeye anasema: Haitoshi tu wewe kuwa mutumishi wangu, kusudi uyainue makabila ya Yakobo, na kurudisha watu wa Israeli waliobaki. Nitakufanya ukuwe mwangaza wa mataifa, kusudi watu wote wapate kuokolewa katika dunia.


Yule mwanamuke akasema: “Ndiyo, Bwana, unasema ukweli, lakini hata imbwa wanazoea kula makombo yanayoanguka chini ya meza ya wabwana wao.”


Mufanye vile kusudi mupate kuwa kweli watoto wa Baba yenu anayekuwa mbinguni. Kwa maana yeye anawaangazia waovu na wema jua lake, naye anawanyeshea mvua wenye haki na wasiokuwa wenye haki.


Lakini Yesu akamujibu: “Uwaache kwanza watoto wa nyumba washibe, kwa sababu si vizuri kukamata chakula cha watoto na kukitupia imbwa.”


Basi Yesu akamwambia: “Kwa sababu ya jibu hili, unaweza kurudi kwako, yule pepo ametoka ndani ya binti yako.”


Basi hakuna tofauti kati ya Wayuda na watu wa mataifa mengine, kwa maana Bwana wa wote ni mumoja tu, na anawabariki sana wote wanaomusihi.


Au Mungu ni Mungu wa Wayuda tu? Yeye si Mungu wa watu wa mataifa mengine vilevile? Ndiyo, yeye ni Mungu wa watu wa mataifa mengine vilevile,


Mimi ni mudogo kuliko watu wote wa Mungu, lakini Mungu amenijalia neema ya kutangaza kwa watu wa mataifa mengine Habari Njema ya baraka za Kristo zisizoweza kuhesabiwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ