Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 7:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Kwa maana ni ndani ya mutu, ni kusema ndani ya moyo wake, ndimo munamotoka mawazo mabaya yanayoleta: uzinzi, wizi, uuaji,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 7:21
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe alipoona uwingi wa uovu wa watu katika dunia, na kwamba kila kitu mwanadamu anachokusudia ndani ya moyo wake ni kiovu siku zote,


Harufu nzuri ya sadaka hiyo ikamupendeza Yawe, naye akasema ndani ya moyo wake: “Sitailaani tena inchi hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu. Ninajua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe vyote kama vile nilivyofanya.


Nani anayeweza kutoa kitu kisafi kutoka kitu kichafu? Hakuna anayeweza.


Mutu anaweza basi namna gani kuwa mwenye haki mbele ya Mungu? Mwanadamu tu anaweza namna gani kujidai kuwa safi?


Uvute moyo wangu kufuata maagizo yako, na si kwa ajili ya kupata faida isiyofaa.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi. Mupumbafu anajisemesha hivi katika moyo: “Hakuna Mungu.” Wote wamepotoka kabisa, matendo yao ni ya kuchukiza; hakuna hata mumoja anayetenda mazuri!


Lakini wote wamekosa, wote wamepotoka pamoja; hakuna anayetenda mazuri, hakuna hata mumoja.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo wa huzuni. Mashairi ya Daudi.


Mungu anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni, aone kama kuna yeyote mwenye akili kama kuna yeyote anayemutafuta Mungu.


Yawe anabomoa makao ya wenye kiburi, lakini analinda mipaka ya makao ya mujane.


Linda moyo wako kwa uangalifu wote, maana mule munatokea chemichemi za uzima.


Tumekuasi na kukukana, ee Yawe, tumekataa kukufuata, ewe Mungu wetu. Tunasema maneno ya kutesa na uasi, katika mioyo yetu tunatunga na kutoa maneno ya uongo.


Muko mbio kutenda maovu, muko wepesi kumwanga damu isiyokuwa na kosa. Mawazo yenu ni mawazo ya uovu, popote munapokwenda munaacha ukiwa na uharibifu.


Ninyi mumefanya vibaya zaidi kuliko babu zenu, maana kila mumoja wenu ni mwenye moyo mugumu na mwenye nia mbaya, wala hamunisikilizi.


Moyo wa mutu ni mudanganyifu kuliko vitu vyote; hauwezi kuponyeshwa, hakuna anayeweza kuuelewa!


Wewe Yerusalema, usafishe maovu ya moyo wako, kusudi upate kuokolewa. Mpaka wakati gani utaendelea kuchunga maovu?


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ile, utaanza kuwaza ndani ya moyo wako na kupanga mipango miovu na kusema:


Kwa maana ndani ya moyo munatoka mawazo mabaya yanayoleta uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushuhuda wa uongo na matukano.


Naye Yesu akijua mafikiri yao, akawauliza: “Sababu gani munawaza maneno hayo mabaya?


Yesu akaongeza kusema: “Ni kile kinachotoka ndani ya mutu ndicho kinachomuchafua.


uasherati, tamaa mbaya, matendo mabaya, ukorofi, maisha ya ovyo, wivu, matukano, majivuno na upumbafu.


Yesu akawaambia: “Ninyi ni watu wanaojionyesha kuwa wenye haki mbele ya watu, lakini Mungu anajua yanayokuwa ndani ya mioyo yenu. Kwa maana mambo yanayosifiwa na watu ni machukizo mbele ya Mungu.


Mbele haujauzisha lile shamba, si lilikuwa mali yako? Na nyuma ya kuliuzisha, feza ulizopata haungezitumia sawa unavyotaka? Basi namna gani ulikusudia kufanya jambo kama hili? Haukusema uongo mbele ya watu, lakini mbele ya Mungu!”


Basi ugeuke toka katika zambi zako na umwombe Bwana, labda atakusamehe kwa ajili ya mawazo ya namna hii.


Kwa maana tulipoishi maisha ya kimwili, tamaa ya kufanya zambi iliyotokana na Sheria ilitumika ndani yetu na kutuletea kifo.


Kutokana na amri, zambi ilipata njia hata kuamusha kila namna ya tamaa ndani yangu. Kwa maana pasipo Sheria zambi ingekuwa kama mufu.


Basi mutupilie mbali mambo yote ya kidunia yanayokuwa ndani yenu: uasherati, uchafu, nia mbaya, tamaa mbaya na tamaa ya mali inayokuwa sawa vile kuabudu sanamu.


Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.


Jambo hilo halionyeshi kwamba munafanya ubaguzi, na kwamba kwa kuamua vile munaongozwa na mawazo mabaya?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ