Kuna taifa ambalo limekwisha kubadilisha miungu yao ingawa miungu hiyo si miungu? Lakini watu wangu wameniacha mimi, utukufu wao, wakafuata miungu isiyokuwa na faida yoyote.
Yesu alizunguka katika Galilaya yote akifundisha katika nyumba zao za kuabudia, akihubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha watu waliokuwa na magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.
Yesu aliposikia maneno haya, akashangaa na kuwaambia watu waliomufuata: “Kweli ninawaambia: katika inchi yote ya Israeli, sijaona bado mutu anayekuwa na imani kubwa kama huyu.
Yesu alizunguka katika miji na vijiji vyote, akiwafundisha watu katika nyumba zao za kuabudia, akiwahubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.
Yesu akaondoka kule, akaenda katika jimbo la Yudea na kuvuka ngambo ingine ya Yordani. Na makundi mengi ya watu wakakusanyika tena mbele yake, naye akaanza kuwafundisha, kama vile alivyozoea kufanya.
Tena ninyi munajua namna Mungu alivyomuchagua Yesu wa Nazareti kwa kazi yake, akimujaza na Roho Mutakatifu na kumupatia uwezo. Naye alipita fasi zote akitenda mema na kuwaponyesha watu wote waliokuwa chini ya mamlaka ya Shetani. Ilitendeka vile kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.