16 Lakini Herode aliposikia habari zile, akasema: “Ni yule Yoane Mubatizaji niliyemukata kichwa ndiye amefufuka!”
Hao wanaotenda maovu hawajui kitu? Wanatafuna watu wangu kama mikate; wala hawajali Mungu.
Halafu akawaambia wasimamizi waliokuwa chini yake: “Mutu huyu ni Yoane Mubatizaji aliyefufuka! Ni kwa sababu hii amepata uwezo wa kufanya miujiza.”
Akawaambia: “Nimekosa kwa kumutoa mutu huyu asiyekuwa na kosa auawe.” Lakini wao wakamujibu: “Jambo hilo halituelekei. Ni kazi yako wewe mwenyewe!”
Lakini wengine walisema: “Huyu ni nabii Elia.” Wengine walisema: “Yeye ni nabii sawa na mumoja wa wale manabii wa zamani.”
Ni Herode mwenyewe aliyeamuru kwamba Yoane akamatwe na kutiwa katika kifungo. Ilitokea vile kwa sababu Herode alimwoa Herodia, muke wa ndugu yake Filipo.
Lakini Herode alisema: “Mimi nimeamuru Yoane akatwe kichwa. Basi huyu ninayesikia habari zake ni nani?” Naye akatafuta namna ya kumwona Yesu.