Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 5:40 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

40 Nao wakaanza kumuchekelea. Halafu Yesu akawaondosha wote inje, akawakamata wazazi wa yule mutoto na wanafunzi wake watatu, akaingia katika chumba pahali mutoto alipokuwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 5:40
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Loti akawaendea wachumba wa wabinti zake, akawaambia: “Haraka! Mutoke pahali hapa, maana Yawe atauangamiza muji huu.” Lakini wao wakamwona kama mutu mwenye kuchekesha tu.


Lakini Sanibalati, Muhori, Tobia, Mwamoni mutumishi wake, na Gesemi, Mwarabu, waliposikia hayo, wakatucheka na kutuzomea wakisema: “Ni kitu gani hiki munachotenda? Munataka kumwasi mufalme?”


Nilikuwa mutu wa kumwomba Mungu na kupata jibu lake. Sasa, watu wananichekelea. Wanachekelea mutu mukamilifu, mwenye haki.


Lakini mimi ni mududu tu, wala si mutu; nimetukaniwa na kuzarauliwa na watu.


Kitu kinachoingia ndani ya kinywa cha mutu hakiwezi kumuchafua. Lakini ni kile kinachotoka ndani ya kinywa chake ndicho kinachomuchafua.”


“Musiwape imbwa vitu vitakatifu, kusudi wasiwageukie na kuwararua, wala musiwatupie nguruwe ushanga zenu za bei kusudi wasizikanyagekanyage.


Akaingia ndani ya nyumba, akawaambia: “Kwa nini munafanya makelele na kulia? Mutoto hakukufa, lakini analala tu!”


Akashika mukono wa mutoto, akamwambia: “Talita kumu,” maana yake: “Kijana binti, ninakuambia, amuka!”


Wakati Wafarisayo waliposikia maneno haya yote wakamuzarau Yesu, kwa sababu walikuwa wapenda feza.


Nao waliposikia Paulo akisema juu ya ufufuko, wamoja wakamuchekelea na wengine wakasema: “Tutakusikiliza tena ukisema juu ya habari hii siku ingine.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ