Marko 5:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
23 akamusihi sana, akisema: “Binti yangu mudogo yuko karibu kufa. Ninakuomba ukuje kwanza kwa kuweka mikono yako juu yake, kusudi apate kupona na kuishi!”
Lakini Namani alikasirika sana, akaenda zake akisema: “Nilizani kwamba hakika atanifikia na kumwomba Yawe, Mungu wake, apitishe mikono yake juu ya pahali ninapogonjwa na kuniponyesha!
Yesu akashika mukono wa yule kipofu na kumupeleka inje ya kijiji. Yesu alipokwisha kupakaa mate kwa macho ya mutu yule na kuweka mikono juu yake, akamwuliza: “Unaona kitu?”
Yesu akatoka ndani ya ile nyumba ya kuabudia, akaenda kwa nyumba ya Simoni. Mama mukwe wa Simoni alikuwa ameshikwa na homa kali, halafu wakamwomba Yesu amuponyeshe.
Alipokaribia kwenye mulango wa ukuta wa muji, kukatokea watu wanaobeba maiti ya kijana mumoja aliyekuwa mutoto wa pekee wa mama mumoja mujane. Nao watu wengi wa muji ule walikuwa wakimusindikiza yule mama.
Baba ya Publio alikuwa amelala kwa ajili ya kuwezwa na ugonjwa wa homa na wa kuhara damu. Paulo akaenda kumwangalia, akamwombea na kuweka mikono juu yake, naye akapona.
Basi Anania akaenda. Alipofika ndani ya nyumba ambamo Saulo alikuwa, akaweka mikono juu yake na kumwambia: “Ndugu Saulo, Bwana Yesu aliyekutokea katika njia ulipokuwa ukikuja huku, amenituma kusudi upate kuona tena na kujazwa na Roho Mutakatifu.”