Yesu alianza kufundisha tena pembeni ya ziwa la Galilaya. Kundi kubwa la watu walikusanyika karibu naye, kwa hiyo akaingia ndani ya chombo na kuikaa mule. Chombo kilikuwa katika ziwa na watu walisimama inchi kavu, pembeni ya ziwa.
Yesu alipotoka ndani ya chombo, akakutana na mutu mumoja kule katika muji aliyeshikwa na pepo. Mutu yule hakuvaa nguo tangu siku nyingi, wala hakuishi ndani ya nyumba, lakini aliishi kwenye makaburi.
Yule mutoto alipokuwa akijongea karibu na Yesu, yule pepo akamutupa chini na kumutikisa kwa nguvu. Lakini Yesu akamukaripia yule pepo na kumuponyesha mutoto. Kisha akamurudisha kwa baba yake.