Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 5:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Walipomufikia Yesu, wakamwona yule aliyekuwa na kundi la pepo ndani yake akiikaa, akiwa amevaa nguo nayo akili yake ikiwa sawa. Basi watu wale wakaogopa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 5:15
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku hiyo Daudi akamwogopa Mungu, akasema: “Sasa, nitaweza namna gani kupeleka Sanduku la Agano katika nyumba yangu?”


Kwa sababu hamukulibeba safari ya kwanza, Yawe, Mungu wetu, akatuazibu maana hatukulitunza kama vile alivyoagiza.”


Utukufu wake hauwatishi? Hamupatwi na hofu juu yake?


Hapo watashikwa na hofu, maana Mungu ni pamoja na watu wa haki.


“Hakuna mutu anayeweza kuingia ndani ya nyumba ya mwenye nguvu na kunyanganya vitu vyake, isipokuwa kwanza anamufunga. Na kisha anaweza kunyanganya vitu vyake vyote.


Haujui kwamba ninaweza kumwomba Baba yangu musaada na mara moja angenitumia zaidi ya makundi kumi na mawili ya wamalaika?


Habari zake zikavuma katika inchi yote ya Suria. Wakamuletea watu wote walioteswa na magonjwa mbalimbali na wenye maumivu ya kila namna, wenye pepo, wenye kifafa na wenye kupooza, naye Yesu akawaponyesha.


Wakati Yesu alipokwisha kumufukuza yule pepo, yule bubu akaanza kusema. Nao watu wote wakashangaa na kusema: “Hatujaona jambo kama hili katika inchi yote ya Israeli!”


Wachungaji wa nguruwe wakaenda mbio kupasha habari katika muji na katika vijiji. Watu wakakuja kusudi waone jambo lililotokea.


Nao walioona yale yaliyotendeka wakawaelezea watu wale mambo yaliyomutokea yule aliyekuwa na pepo na yaliyotokea nguruwe.


Yesu alipokuwa akiingia katika chombo, yule aliyekuwa na pepo akamusihi aende pamoja naye.


Mara nyingi miguu yake ilifungwa vifungo vya chuma, nayo mikono yake na minyororo, lakini alikata minyororo ile na kuvunjavunja vile vifungo vya chuma. Hakuna mutu aliyekuwa na nguvu ya kumushinda.


Basi Yesu akamwuliza: “Jina lako nani?” Naye akamujibu: “Jina langu ni ‘Jeshi’, maana sisi ni wengi.”


Marta alikuwa na dada yake mudogo aliyeitwa Maria. Huyo aliikaa mbele ya Bwana, akisikiliza mafundisho yake.


Yesu alipotoka ndani ya chombo, akakutana na mutu mumoja kule katika muji aliyeshikwa na pepo. Mutu yule hakuvaa nguo tangu siku nyingi, wala hakuishi ndani ya nyumba, lakini aliishi kwenye makaburi.


Kwa maana yeye ametuokoa toka katika uwezo wa giza, na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mupendwa,


Kwa maana Mungu hakutupatia sisi Roho wa kuogopa, lakini Roho anayetupatia nguvu, upendo na kujizuiza.


Samweli akafanya sawa alivyoambiwa na Yawe, akaenda Betelehemu. Wazee wa muji wakatoka kwenda kumupokea wakiwa wanatetemeka, wakamwuliza: “Umekuja kwa amani?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ