Yawe akamwambia Shetani: “Basi, unaweza kufanya vile unavyotaka juu ya mali yake. Lakini tu yeye mwenyewe usimuguse.” Basi, Shetani akaondoka mbele ya Yawe.
Mara moja upepo mukali ukavuma kutoka katika jangwa, ukaipiga nyumba ile kila upande nayo ikawaangukia, na vijana wote wamekufa. Ni mimi tu peke yangu nimepona kwa kuja kukuletea habari.”
Yesu alikuwa upande wa nyuma wa chombo, akilala usingizi akilalisha kichwa juu ya mufuko wa kuegemea. Wanafunzi wake wakamwamusha na kumwambia: “Mwalimu, haikuhangaishi kuona sisi tunakufa?”
Lakini wakakwama kwenye lundo ya muchanga na chombo kikakwama pale. Sehemu ya mbele ya chombo ikazama kabisa pasipo kutikisika, lakini sehemu ya nyuma ikavunjikavunjika kwa kupigwa na zoruba kwa nguvu.
Waroma wamenipiga fimbo mara tatu na mara moja walitaka kuniua kwa kunitupia mawe. Mara tatu chombo nilichosafiri nacho kilizama kwa kuvunjika. Mara moja, nilishinda ndani ya bahari kwa muda wa siku nzima.