4 Kisha akawauliza: “Sheria inaturuhusu kufanya mema au kufanya mabaya kwa siku ya Sabato? Kuponyesha mutu au kumwua?” Lakini wakakaa kimya.
Maana kitu ninachotaka kwenu ni wema na si sadaka, kumujua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto.
Halafu Yesu akamwambia yule mwenye mukono unaokauka: “Simama hapa katikati.”
Yesu akawakazia macho kwa kasirani, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wao. Akamwambia yule mutu: “Nyoosha mukono wako.” Akaunyoosha, nao ukakuwa muzima tena.
Lakini wakanyamaza, kwa sababu walikuwa wakibishana katika njia kwamba nani anayekuwa mukubwa kati yao.
Kisha Yesu akawaambia: “Ninawauliza: Sheria inaturuhusu kufanya mema au mabaya kwa siku ya Sabato? Kuponyesha mutu au kumwua?”