Lakini mutu yule alipoenda, akaanza kutangaza habari zile fasi zote. Na kwa sababu hii Yesu hakuweza kuingia tena waziwazi katika muji wowote, lakini alibaki mbali nayo pahali penye ukiwa. Na watu walimufikia kule kutoka pande zote.
Watu waliomufikia Yesu na kuondoka walikuwa wengi sana hata yeye na wanafunzi wake hawakupata wakati wa kula. Kwa sababu hii aliwaambia wanafunzi: “Twende peke yetu kwa pahali penye ukiwa kusudi mupumzike kidogo.”
Yesu akashuka toka kilima pamoja na wanafunzi wake, na kusimama kwenye uwanja. Pale kulikuwa wanafunzi wake pamoja na kundi kubwa sana la watu waliotoka Yerusalema, katika Yudea yote na pande za miji Tiro na Sidona pembeni ya bahari.