Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 3:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Watu waliokuwa na magonjwa walikuwa wakisukumana kusudi wamufikie na kumugusa kwa maana aliwaponyesha watu wengi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 3:10
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Yawe akamutesa na watu wote wa nyumba yake kwa mapigo makali kwa sababu ya Sarai, muke wa Abramu.


Kulikuwa kungali nyama kwa wingi na mbele watu hawajawamaliza kula, Yawe akawakasirikia watu, akawapiga watu kwa pigo kubwa sana.


Yesu alipojua habari ile, akaondoka kule. Watu wengi wakamufuata, naye akawaponyesha wagonjwa wote.


Yesu alipotoka ndani ya chombo, akaona kundi kubwa la watu, naye akawasikilia huruma, akawaponyesha wale waliokuwa wagonjwa kati yao.


na kumusihi awaruhusu waguse hata upindo wa nguo yake tu. Nao wote waliougusa walipona.


Yesu alizunguka katika Galilaya yote akifundisha katika nyumba zao za kuabudia, akihubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha watu waliokuwa na magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.


Yesu akamwambia: “Binti yangu, imani yako imekuponyesha. Ujiendee na amani, ugonjwa wako umepona!”


Na kila pahali Yesu alipokwenda, katika vijiji, miji, au kwenye mbuga, watu waliweka wagonjwa katika viwanja vya makutano na kumusihi awaache wagonjwa waguse hata upindo wa kanzu yake tu. Nao wote waliougusa, walipona.


Yesu na wanafunzi wake wakafika Betesaida. Kule wakamuletea Yesu mutu mumoja kipofu na kumwomba amuguse kusudi apate kupona.


Yesu akaingia ndani ya moja kati ya vile vyombo, nacho kilikuwa cha Simoni. Yesu akamwomba akisukume mbali kidogo na kivuko. Halafu akaikaa mule na kuwafundisha watu.


Watu wote walitaka kumugusa, kwa sababu uwezo ulikuwa ukitoka ndani yake na kuwaponyesha wote.


Kule kulikuwa mukubwa mumoja wa waaskari aliyekuwa na mutumishi wake mupendwa sana. Mutumishi yule alikuwa mugonjwa karibu kufa.


Saa ile ile Yesu akawaponyesha watu wengi walioteswa na magonjwa na ulema mbalimbali pamoja na wenye pepo, na kuwaponyesha hata vipofu wengi.


Na kufuatana na mambo yote yaliyotokea, watu waliwapeleka wagonjwa katika barabara, wakiwalalisha juu ya mikeka na vipoyi kusudi Petro atakapopita, kivuli chake kipate tu kufika kwenye wamoja wao.


Kwa maana, Bwana anamwazibu yule anayemupenda, yeye anamupiga kila mutu anayemukubali kuwa mutu wake.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ