Malaika akamwambia: “Usinyooshe mukono wako juu ya kijana wala usimufanyie jambo lolote! Sasa ninajua kwamba unamwogopa Mungu, maana haukuninyima hata mwana wako wa pekee.”
Mungu anasema: Kisha kutaabika sana, mutumishi wangu atafurahi. Kwa njia ya kujulikana kwa huyo mutumishi wangu wa haki, atawafanya wengi wakuwe wenye haki, naye atazibeba zambi zao.
Na kule wakamuletea mutu mwenye ugonjwa wa kupooza, akilala juu ya kipoyi. Yesu alipoona namna watu wale walivyomwaminia, akamwambia yule mwenye kupooza: “Mutoto wangu, ujipe moyo! Zambi zako zimesamehewa!”
Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.
Mungu alimupa utukufu na kumwikalisha na mamlaka karibu naye na kumuweka kuwa Mutawala na Mwokozi. Na hivi Waisraeli wataweza kugeuka toka zambi zao na Mungu atawasamehe.
Wakati munaposamehe mutu, nami ninamusamehe vilevile. Kwa maana kama ninasamehe, na ikiwa kweli ninakuwa na neno lolote la kusamehe, ninasamehe mbele ya Kristo kwa ajili yenu,
Muvumiliane na kusameheana ninyi kwa ninyi wakati wowote mutu anapokuwa na neno la kumushitaki mwingine. Munapaswa kusameheana kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi.