Lakini mutu yule alipoenda, akaanza kutangaza habari zile fasi zote. Na kwa sababu hii Yesu hakuweza kuingia tena waziwazi katika muji wowote, lakini alibaki mbali nayo pahali penye ukiwa. Na watu walimufikia kule kutoka pande zote.
Wakati Yesu alipotoka ndani ya chombo, akaona kundi kubwa la watu, akawasikilia huruma, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasiokuwa na muchungaji. Basi akaanza kuwafundisha maneno mengi.
Wakati ule ule makundi mengi ya maelfu ya watu walikusanyika hata wakakanyaganakanyagana. Yesu akaanza kwanza kusema na wanafunzi wake, akiwaambia: “Mufanye angalisho na chachu ya Wafarisayo, maana yake unafiki wao.
Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha, Wafarisayo na walimu wakubwa wa Sheria waliotoka katika kila kijiji cha jimbo la Galilaya na la Yudea na toka Yerusalema, walikuwa wakiikaa pale. Naye alikuwa akiponyesha wagonjwa kwa uwezo wa Bwana.
Nyuma ya pale Yesu akapita katika miji na vijiji mbalimbali, akihubiri na kutangaza Habari Njema ya Ufalme wa Mungu. Wale wanafunzi wake kumi na wawili walienda naye
Nyuma ya kuuawa kwa Stefano, wanafunzi walisambaa kwa ajili ya mateso. Nao wakasafiri mpaka katika inchi ya Foinikia na ya Kipuro na kufika katika muji Antiokia. Na kule walihubiri Neno la Mungu, lakini kwa Wayuda peke yao tu.
Paulo na wale waliomusindikiza wakapita katika inchi ya Furigia na ya Galatia kwa sababu Roho Mutakatifu alikuwa amewakataza wasihubiri Neno la Mungu katika jimbo la Azia.
Lakini inasemwa namna gani? “Neno la Mungu liko karibu nawe, liko ndani ya kinywa chako na ndani ya moyo wako.” Neno hili ni ujumbe tunaouhubiri juu ya imani.