Lakini mutu yule alipoenda, akaanza kutangaza habari zile fasi zote. Na kwa sababu hii Yesu hakuweza kuingia tena waziwazi katika muji wowote, lakini alibaki mbali nayo pahali penye ukiwa. Na watu walimufikia kule kutoka pande zote.
Kisha Yesu akaondoka pale, na kwenda katika jimbo lililokuwa karibu na muji Tiro. Akaingia ndani ya nyumba, naye hakutaka mutu ajue kwamba yuko mule, lakini haikuwezekana kwake kujificha.
Yesu akawaambia: “Hakika mutaniambia fumbo hili: ‘Muganga, ujiponyeshe wewe mwenyewe!’ Na vilevile mutaniambia hivi: ‘Tumesikia mambo yote uliyotenda katika muji Kapernaumu, basi uyafanye hapa vilevile katika muji wako.’ ”
Wakati aliposikia kwamba Yesu amefika Galilaya toka Yudea, mukubwa huyu akamwendea, akamusihi aende Kapernaumu kumuponyesha mwana wake, aliyekuwa karibu kufa.
Wakati waliposikia ile fujo, wakakusanyika kwa uwingi. Wote wakapigwa na mushangao, kwa sababu kila mumoja wao aliwasikia waamini wakisema katika luga yake ya kuzaliwa.