7 Muende sasa kupasha habari kwa wanafunzi wake na kwa Petro, muwaambie kwamba anawatangulia Galilaya; nao watamwona kule sawa vile alivyowaambia.”
Lakini nitakapokwisha kufufuka, nitawatangulia Galilaya.”
Kisha Yesu akawaambia: “Musiogope, muende kuwaambia wandugu zangu waende Galilaya, na kule wataniona.”
Muende upesi kuwaambia wanafunzi wake kwamba amefufuka, naye anawatangulia Galilaya, ni kule watakapomwona. Basi, nimekwisha kuwaambia ninyi.”
Wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.
Basi walitoka kwenye kaburi na kukimbia mbio. Walikuwa wakitetemeka na kushangaa sana. Nao hawakumwambia mutu yeyote, kwa sababu waliogopa. [
Nyuma ya mambo hayo, Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kandokando ya ziwa la Tiberia. Angalia sasa namna alivyowatokea:
Na kwa siku nyingi akaonekana kwa waliosafiri pamoja naye toka Galilaya kwenda Yerusalema. Na wale ndio sasa wanaomushuhudia mbele ya watu.
Alimutokea Petro, na kisha akawatokea mitume wake kumi na wawili.
Basi sasa ni afazali kumusamehe na kumufariji, na kuepuka asikate kitumaini kwa sababu ya huzuni kubwa.