Pilato akashangaa sana kusikia kwamba Yesu amekwisha kufa. Basi akamwita yule mukubwa wa waaskari na kumwuliza kama kumepita muda murefu tangia Yesu alipokufa.
Yosefu akanunua vitambaa, akaondoa maiti ya Yesu juu ya musalaba, akaifungafunga na vile vitambaa na kuiweka ndani ya kaburi lililochimbwa ndani ya jiwe. Kisha wakasukumia jiwe kwenye kiingilio cha lile kaburi.
Nyuma ya mambo hayo, Yosefu, mutu wa Arimatea, akamwomba Pilato ruhusa ya kuondoa maiti ya Yesu. (Yosefu alikuwa mumoja wa wanafunzi wa Yesu lakini kwa siri, kwa sababu aliwaogopa wakubwa wa Wayuda.) Pilato akamuruhusu. Basi Yosefu akaenda na kuondoa maiti ya Yesu.