Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 15:40 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

40 Kulikuwa wanawake wamoja walioangalia kwa mbali. Kati yao kulikuwa Maria wa Magdala, Maria mama ya kijana Yakobo na Yose na mwanamuke mwingine Salome.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 15:40
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Moyo wangu unapigapiga, nguvu zimeniishia; hata macho yangu nayo yamekwisha fifia.


kisha Filipo na Bartolomayo, Toma na Matayo aliyekuwa mulipishaji wa kodi; Yakobo mwana wa Alfayo, na Tadeo;


Huyu si mwana wa yule seremala? Mama yake si Maria? Nao Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda si wandugu zake?


Maria wa Magdala na yule Maria mwingine walikuwa wakiikaa pale, kuelekea kwenye kaburi.


Siku ya Sabato ilipokwisha kupita, kesho yake siku ya kwanza ya juma, kwa wakati wa mapambazuko, Maria wa Magdala na Maria mwingine wakaenda kuangalia kaburi.


Maria wa Magdala na Maria mama ya Yose walikuwa wakiangalia, pahali walipomuzika Yesu.


Siku ya Sabato ilipokwisha kupita, Maria wa Magdala, na Maria mama ya Yakobo, na mwanamuke mwingine Salome, walinunua marasi kusudi waende kupakaa maiti ya Yesu.


Yesu alipokwisha kufufuka asubui mapema, siku ya kwanza ya juma, alimutokea kwanza Maria wa Magdala, yule aliyefukuza pepo saba toka ndani yake.


Alitaka kuona Yesu ni nani, lakini kwa vile alivyokuwa mutu mufupi, hakuweza kumwona kwa sababu watu walikuwa wengi.


Na wote waliojuana sana naye, na hata wanawake waliomufuata tangia Galilaya, walisimama kwa mbali wakiangalia mambo hayo.


Au sina haki ya kusafiri pamoja na mwanamuke mukristo kama vile mitume wengine wanavyofanya, nao wandugu za Bwana na hata Petro?


Sikumwona mutu mwingine isipokuwa tu Yakobo, ndugu ya Bwana.


Barua hii inatoka kwangu mimi Yakobo, mutumishi wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo. Ninawasalimia ninyi watu wa makabila kumi na mawili waliosambazwa katika dunia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ