Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 15:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Mutu mumoja wa Kurene, aliyeitwa Simoni, baba ya Alesanduro na Rufu, alikuwa akipita katika njia, akitoka kwenye vijiji. Waaskari wakamushurutisha abebe musalaba wa Yesu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 15:21
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walipokuwa wakiondoka, wakamwona mutu mumoja wa Kurene, aliyeitwa Simoni; wakamushurutisha abebe musalaba wa Yesu.


Kama mutu anayetumwa na wakubwa akikulazimisha kubeba muzigo kilometre moja, uubebe hata kilometre mbili.


Walipokwisha kumuchekelea, wakamuvua ile nguo nyekundu na kumuvalisha nguo zake. Kisha wakaondoka naye inje kwa kwenda kumutundika juu ya musalaba.


Mutu yeyote asiyejitolea kwa kubeba musalaba wake na kunifuata, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.


Nao walipokuwa wakimupeleka Yesu kwenda kutundikwa, wakakutana na mutu mumoja aliyeitwa Simoni, wa inchi ya Kurene, aliyekuwa akitoka kwenye vijiji. Wakamulazimisha abebe musalaba wa Yesu na kumufuata nyuma.


Yesu akaondoka katika muji akibeba musalaba wake mpaka kwenye nafasi inayoitwa katika Kiebrania “Golgota”, maana yake: “Kilima cha Mufupa wa Kichwa.”


Lakini kulitokea wanafunzi wengine, waliokuwa watu wa Kipuro na wa inchi ya Kurene, waliofika Antiokia. Nao wakaanza kusemezana na Wagriki vilevile, wakiwahubiri Habari Njema juu ya Bwana Yesu.


Katika kanisa la Antiokia kulikuwa manabii na walimu wamoja. Kati yao kulikuwa Barnaba, Simoni aliyeitwa vilevile Nigeri; Lukio wa Kurene, Saulo na Manaeni, aliyekomaa pamoja na mufalme Herode.


Furigia, Pamfilia, Misri na pande za Libya karibu na Kurene. Vilevile kuna wageni waliotoka Roma,


Lakini kukatokea watu wamoja waliopingana na Stefano. Watu hawa walikuwa wa nyumba ya kuabudia iliyojulikana kwa jina la “Wenye Uhuru.” Nao walitoka katika inchi ya Kurene na ya Alesanduria, na kutoka jimbo la Kilikia na la Azia. Watu hawa wakaanza kubishana na Stefano


Munisalimie Rufo, mutumishi hodari katika kazi ya Bwana, na mama yake ninayemuhesabu kama mama yangu vilevile.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ