Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 14:61 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

61 Lakini Yesu akanyamaza, wala hakujibu neno. Kuhani Mukubwa akamwuliza tena: “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu mwenye sifa?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 14:61
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Utukuzwe, ee Yawe! Unifundishe masharti yako.


Mufalme anasema: “Nitatangaza amri ya Yawe. Mungu aliniambia: ‘Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.


Uniokoe katika makosa yangu yote; usikubali wapumbafu wanichekelee.


Alionewa na kuteswa, lakini alivumilia kwa unyenyekevu, bila kutoa sauti hata kidogo. Alikuwa kama mwana-kondoo anayepelekwa kwenda kuchinjwa, kama kondoo anavyokaa kimya anapokatwa manyoya. Hakutoa sauti hata kidogo.


Simoni Petro akamujibu: “Wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu Mwenye Uzima.”


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


Halafu wakaanza kulalamika wakisema: “Kuna maneno gani kati yako na sisi wewe Mwana wa Mungu? Umekuja hapa kwa kututesa mbele ya kutimia kwa wakati wetu?”


Basi Kuhani Mukubwa akasimama katikati ya watu na kumwuliza Yesu: “Haujibu hata neno? Watu hawa wanakushitakia nini?”


Pilato akamwuliza Yesu: “Wewe ni Mufalme wa Wayuda?” Yesu akamujibu: “Umesema.”


Mimi nimeona mambo haya, nami ninashuhudia kwamba huyu ndiye Mwana wa Mungu.”


Halafu Wayuda wakamuzunguka, na kumwambia: “Mpaka wakati gani utatuzungusha kichwa? Kama wewe ni Kristo, utuambie waziwazi.”


Kwa upande wangu, nilichaguliwa na Mungu na kutumwa naye katika dunia. Basi namna gani munasema kwamba ninamutukana Mungu kwa sababu nilisema kwamba mimi ni Mwana wa Mungu?


Halafu Pilato akamwuliza: “Ni kusema wewe ni mufalme?” Yesu akamujibu: “Wewe umesema kwamba mimi ni mufalme. Mimi nimezaliwa na kuja katika dunia kusudi nishuhudie ukweli. Wote wanaokuwa upande wa ukweli, wananisikiliza mimi.”


Wayuda wakamujibu: “Kufuatana na moja ya sheria zetu, mutu huyu anapaswa kuuawa, kwa sababu alijiita Mwana wa Mungu.”


Akaingia tena katika nyumba yake na kumwuliza Yesu: “Wewe ni muzaliwa wa wapi?” Lakini Yesu hakumujibu neno.


Na sehemu ya Maandiko aliyokuwa akisoma ni hii: “Alipelekwa kama kondoo kwenda kuchinjwa, kama mwana-kondoo anayenyamaza mbele ya mwenye kumukata manyoya. Yeye hakufungua kinywa chake.


Mafundisho haya yanalingana na Habari Njema ya utukufu wa Mungu mwenye baraka, ambayo nilipewa nipate kuihuburi.


Kutokea kwake kutafanywa na Mungu kwa wakati aliopanga. Yule ndiye Mungu anayestahili kutukuzwa, anayekuwa peke yake mutawala, mufalme wa wafalme na Bwana wa wabwana.


Wakati walipomutukana, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutisha watu hata wamwogope. Lakini alijiachilia katika mikono ya Mungu anayehukumu watu kwa haki.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ