Basi, Elia aliposikia sauti hiyo, alijifunika uso kwa koti lake, akatoka na kusimama kwenye mulango wa pango. Halafu, akasikia sauti: “Elia! Unafanya nini hapa?”
Lakini Petro akamufuata Yesu kwa mbali, hata akaingia ndani ya upango wa Kuhani Mukubwa. Akaingia katika kiwanja, akaikaa pamoja na walinzi kusudi aone mambo yatakayotokea.
Watumishi na walinzi walikuwa wamekonga moto kwa sababu wakati ule ulikuwa wa baridi, nao walisimama pale wakiota moto. Petro alisimama pale vilevile, akiota moto pamoja nao.
Wakati ule Simoni Petro alikuwa angali pale akiota moto. Basi wakamwuliza: “Wewe vilevile si mumoja wa wanafunzi wa mutu huyu?” Petro akakana, akisema: “Hapana! Mimi si mwanafunzi wake.”
Wengine walivuka muto Yordani mpaka katika inchi ya Gadi na inchi ya Gileadi. Lakini Saulo alikuwa angali kule Gilgali pamoja na watu wote waliomufuata wakitetemeka.