Marko 14:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
13 Basi Yesu akawatuma wawili kati ya wanafunzi wake akiwaambia: “Mwende katika muji, na kule mutakutana mutu mumoja anayebeba mutungi wenye maji. Mumufuate mutu yule,
Hata mimi vilevile ni mutu mwenye kuwa chini ya mamlaka ya wakubwa, na tena nina waaskari wengine wanaokuwa chini yangu. Nami nikimwambia mumoja: ‘Kwenda!’, naye anakwenda. Nikimwambia mwingine: ‘Kuja!’, naye anakuja. Na nikimwambia mutumishi wangu: ‘Fanya hivi!’, naye anafanya vile.”
Siku ya kwanza ya karamu ya sikukuu ya Mukate Usiyotiwa Chachu, wakati ambapo walichinja kondoo wa Pasaka, wanafunzi wa Yesu wakamwuliza: “Unataka tuende wapi kukutayarishia karamu ya Pasaka?”
na pahali atakapoingia, mumwambie mwenye nyumba: ‘Mwalimu anauliza kwamba ni wapi kunapokuwa chumba chake ambamo atakulia karamu ya Pasaka pamoja na wanafunzi wake.’
Hakuna kitu kinachoweza kufichwa mbele ya Mungu, lakini vitu vyote vinafunuliwa na viko wazi mbele ya macho yake, yeye tutakayemutolea hesabu ya maneno yetu.