Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 14:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Waliposikia habari ile wakafurahi sana, nao wakamwahidia kumupa feza. Basi Yuda akaanza kutafuta wakati muzuri kwa kumutoa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 14:11
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Ahabu alipomwona Elia, akasema: “Ewe adui yangu, umeninasa tena?” Elia akamujibu: “Ndiyo! Nimekunasa, kwa sababu wewe umekusudia kabisa kutenda maovu mbele ya Yawe.


Lakini Elisha akamwambia: “Unafikiri roho yangu haikukuwa pamoja nawe wakati mutu yule alipotoka ndani ya gari lake na kuja kukutana nawe? Huu ndio wakati wa kupokea feza na nguo, mashamba ya mizeituni na mizabibu, kondoo na ngombe au watumishi na wajakazi?


Wanamufurahisha mufalme, lakini ni waovu; wanawafurahisha wakubwa, lakini ni wanafiki.


Halafu mumoja wa wanafunzi kumi na wawili, aliyeitwa Yuda Iskariota, akaenda kwa wakubwa wa makuhani


na kuwaambia: “Mutanipa nini kama nikimutoa Yesu kwenu?” Basi wakamupa vikoroti makumi tatu vya feza.


Yuda Iskariota, mumoja wa wanafunzi kumi na wawili, akaenda kwa wakubwa wa makuhani, kusudi amutoe Yesu kwao.


Siku ya kwanza ya karamu ya sikukuu ya Mukate Usiyotiwa Chachu, wakati ambapo walichinja kondoo wa Pasaka, wanafunzi wa Yesu wakamwuliza: “Unataka tuende wapi kukutayarishia karamu ya Pasaka?”


Basi Shetani akamwingia Yuda, yule anayeitwa Iskariota, aliyekuwa mumoja wa wanafunzi kumi na wawili.


Kwa maana kupenda feza ni shina la mabaya yote. Kwa ajili ya kuzitamani watu wamoja wanaanguka katika imani yao, na wanajiumiza mioyo wakijiletea huzuni nyingi.


Ole kwao! Maana wamefuata njia ya Kaina. Kwa ajili ya kupata mali wameanguka katika kosa Balama alilofanya. Wameangamia kwa sababu wameasi kama vile Kora alivyoasi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ