Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 13:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 “Mujiangalie vizuri ninyi wenyewe, kwa maana watawapeleka mbele ya tribinali kwa kuwahukumu na kuwapiga fimbo katika nyumba za kuabudia. Vilevile mutapelekwa mbele ya wakubwa na wafalme kwa ajili yangu, kusudi mutoe ushuhuda wangu mbele yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 13:9
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayemukasirikia ndugu yake anapaswa kuhukumiwa. Naye anayemwambia ndugu yake: ‘Hauna akili wewe!’ anapaswa kupelekwa kwenye tribinali kubwa. Naye anayemwambia: ‘Uko mwenda-wazimu!’ anastahili kutupwa katika jehenamu.


“Angalisho, usimwambie mutu hata neno moja juu ya hii. Lakini kwenda kwa kuhani na kumwonyesha jinsi unavyokuwa sasa. Kisha utoe sadaka kama Musa alivyoamuru, kuwa ushuhuda kwa wote kwamba umetakaswa.”


Basi Yesu akaanza kuwaambia: “Muangalie vizuri mutu asiwadanganye.


Kwa maana taifa litapigana na taifa, na ufalme utapigana na ufalme. Kutakuwa tetemeko la inchi pahali mbalimbali. Vilevile kutakuwa njaa. Na haya yote ni kama mwanzo wa maumivu ya kuzaa tu.


Na nafasi yoyote watu watakapokataa kuwakaribisha na kuwasikiliza, mutoke kule na mukungute mavumbi toka juu ya miguu yenu. Jambo hili litakuwa ushuhuda juu yao.”


Na katika muji wowote watu watakapokataa kuwakaribisha, mutoke kule na mukungute mavumbi toka juu ya miguu yenu. Jambo hili litakuwa ushuhuda juu yao.”


Mukumbuke maneno niliyowaambia kwamba mutumishi si mukubwa kuliko bwana wake. Kama walinitesa mimi, watawatesa ninyi vilevile. Na kama walishika maneno yangu, watashika maneno yenu vilevile.


Watawatenga musiingie katika nyumba za kuabudia. Na kutakuwa wakati ambapo wote watakaowaua watazani kwamba wanamutumikia Mungu.


Akatufikia, akatwaa mukaba wa Paulo, akajifunga miguu na mikono yake mwenyewe na kusema: “Roho Mutakatifu anasema: ‘Wayuda watamufunga mutu mwenye mukaba huu namna hii kule Yerusalema na kumutoa kwa watu wa mataifa mengine.’ ”


Wajumbe wa Baraza Kubwa waliposikia maneno hayo, wakakasirika sana na kumusagia Stefano meno.


Nami nitamwonyesha mateso ya namna gani atakayopaswa kupata kwa ajili yangu.”


Kwa maana Mungu amewapa ninyi neema ya kumutumikia Kristo, na si kwa kumwamini tu, lakini vilevile kwa kuteswa kwa ajili yake.


Hayo yote yanahakikisha kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki na matokeo yake ni kwamba ninyi munastahili kuingia katika Ufalme wake ambao kwa ajili yake ninyi munateseka.


Basi, mujiangalie wenyewe, kusudi musipoteze matunda ya kazi yenu, lakini mupokee zawadi kamili.


Mimi ni ndugu yenu Yoane. Kwa njia ya kuungana na Yesu, ninashirikiana nanyi katika mateso, katika ufalme wake na katika kuvumilia. Mimi nilikuwa nimepelekwa katika kisanga kinachoitwa Patimo, kwa sababu nilihubiri Neno la Mungu na ukweli ulioshuhudiwa na Yesu.


Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.


Ninajua pahali pale unapokaa, ile ndiyo nafasi ya utawala wa Shetani. Wewe unashikamana na jina langu, wala haukuikana imani unayokuwa nayo kwangu, hata wakati Antipa, mushuhuda wangu mwaminifu, alipouawa kati yenu kule kwenye makao ya Shetani.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ