Vilevile kwa Siku ya hukumu malkia toka kusini atasimama na watu wa kizazi hiki na kuwashitaki, kwa sababu yeye alitoka mbali sana kuja kusikia maneno ya hekima ya mufalme Solomono. Hapa kuna yule anayekuwa mukubwa kumupita Solomono!
Mwana wa Mutu atawatuma wamalaika wake, nao watakusanya toka katika Ufalme wake watu wote wanaowaangusha wengine katika zambi pamoja na wote wanaofanya maovu.
Na kama Mungu asingepunguza siku zile za mateso, hakuna hata mutu mumoja angeponyoka kufa. Lakini kwa ajili ya watu wake aliowachagua, yeye atazipunguza.
kwa maana kutatokea watu wanaojiita kwa uongo ‘Kristo’ pamoja na manabii wa uongo, nao wataonyesha vitambulisho vikubwa na maajabu, hata ikiwezekana, wawadanganye hata watu waliochaguliwa na Mungu.
Baragumu kubwa itapigwa, halafu atawatuma wamalaika wake katika pande ine za dunia, kusudi wawakusanye watu wake aliowachagua, kutoka katika dunia nzima.
Na kama Bwana asingepunguza siku zile za mateso, hakuna hata mutu mumoja ambaye angeponyoka kufa. Lakini kwa ajili ya wachaguliwa aliowachagua amezipunguza.
Kwa maana kutatokea watu wanaojiita kwa uongo ‘Kristo’ pamoja na manabii wa uongo, nao watafanya vitambulisho na maajabu, kusudi ikiwezekana wawadanganye wachaguliwa wa Mungu.
“Muangalilie mufano juu ya muti wa tini. Wakati matawi yake yanapochipuka, nayo majani yao yanapochipuka, ninyi munatambua kwamba wakati wa jua kali unakaribia.
Ninyi ni watu wa Mungu, yeye amewapenda na kuwachagua kwa ajili yake mwenyewe. Kwa hiyo, mukuwe na moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
Ni kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya watu ambao Mungu alijichagulia kuwa wake, kusudi wao vilevile wapate kuokoka na kupata utukufu wa milele unaopatikana kwa njia ya Kristo Yesu.
Mungu Baba aliwachagua ninyi tangu mbele kufuatana na mupango wake na kufanywa watakatifu na Roho, mupate kumutii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Ninawatakia neema na amani kwa uwingi.