Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 13:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Na halafu wakati ule Mwana wa Mutu ataonekana akikuja katikati ya mawingu kwa uwezo mwingi na kwa utukufu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 13:26
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yesu akamwambia: “Heri kwako, wewe Simoni mwana wa Yona, kwa maana hakuna mutu aliyekufunulia neno hili isipokuwa Baba yangu anayekuwa mbinguni.


Kwa maana Mwana wa Mutu atakuja na wamalaika akitukuzwa na Baba yake, halafu atamulipa kila mutu kufuatana na matendo yake.


Kweli ninawaambia: wamoja kati ya watu wanaokuwa hapa hawatakufa mbele hawajamwona Mwana wa Mutu akikuja katika Ufalme wake.”


Kisha kitambulisho cha kurudi kwa Mwana wa Mutu kitaonekana katika mbingu. Nayo mataifa yote ya dunia yatakuwa katika malalamiko, na yatamwona Mwana wa Mutu akikuja katikati ya mawingu toka mbinguni, kwa uwezo na utukufu mukubwa.


“Wakati Mwana wa Mutu atakapokuja katika utukufu wake pamoja na wamalaika wote, ataikaa juu ya kiti chake cha kifalme chenye utukufu.


Yesu akajibu: “Mimi Ndiye! Nanyi mutamwona Mwana wa Mutu akiikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo. Mutamwona vilevile akikuja katika mbingu katikati ya mawingu!”


Kwa hiyo mutu yeyote anayesikia haya juu yangu na juu ya mafundisho yangu kati ya watu wa kizazi hiki kisichokuwa na uaminifu mbele ya Mungu na chenye zambi, Mwana wa Mutu atasikia haya juu yake vilevile. Itakuwa vile, atakapokuja pamoja na wamalaika watakatifu, akitukuzwa na Baba yake.”


Na Yesu akaongeza kusema: “Kweli ninawaambia: wamoja kati ya watu wanaokuwa hapa hawatakufa mbele hawajaona Ufalme wa Mungu ukikuja kwa uwezo.”


Halafu wakati ule Mwana wa Mutu ataonekana akikuja katikati ya mawingu, kwa uwezo mwingi na kwa utukufu.


Watu hao wakawaambia: “Ninyi Wagalilaya, sababu gani munasimama pale mukiangalia mbinguni? Huyu Yesu aliyenyanyuliwa toka katikati yenu kwenda mbinguni, atarudi sawa vile mulivyomwona akienda.”


Kwa sababu amri itakapotoka na sauti ya malaika mukubwa itakaposikilika, na baragumu ya Mungu itakapolia, Bwana mwenyewe atashuka toka mbinguni. Halafu wale waliokufa wakimwamini Kristo watafufuliwa kwanza.


Basi, wakati tulipowajulisha uwezo na kurudia kwa Bwana wetu Yesu Kristo, sisi hatukutumia hadisi za uongo zilizotungwa kwa werevu. Lakini tulijionea na macho yetu sisi wenyewe uwezo wake.


Angalia, yeye anakuja katikati ya mawingu! Kila mutu atamwona, hata wale waliomutoboa kwa mukuki. Na kwa sababu yake mataifa yote ya dunia yatalalamika kwa huzuni. Hakika ni vile! Amina.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ