Makerubi wakakunjua mabawa yao, wakapanda juu, mimi nikiwa ninawaona na yale magurudumu yalikuwa pembeni yao. Wakasimama mbele ya mulango wa upande wa mashariki wa nyumba ya Yawe, na utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
Utukufu wa Yawe ukapanda juu tokea wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha nyumba hiyo, na lile wingu likaijaza nyumba, na kiwanja kilijaa mwangaza wa utukufu wa Yawe.
Basi, Mungu akaniambia hivi: Wewe mwanadamu, unaona mambo wanayofanya, machukizo makubwa Waisraeli wanayofanya kusudi wapate kunifukuza kutoka katika hekalu langu? Tena utaona machukizo mengine makubwa zaidi.