Basi Yesu akawaita wanafunzi wake na kuwaambia: “Kweli ninawaambia kwamba mujane huyu masikini ametoa mingi zaidi kuliko wote wanaotia feza ndani ya sanduku ya sadaka.
Yule mudogo akamwambia baba yake: ‘Baba, unipe ile sehemu ya urizi inayopaswa kuwa yangu.’ Basi baba akagawanya mali yake kati ya wana wake wote wawili.
Kati yao kulikuwa mwanamuke mumoja mwenye ugonjwa wa kutokwa na damu kwa muda wa miaka kumi na miwili. Alikuwa ametumia mali yake yote kwa kulipa waganga, lakini hakuna hata mumoja wao ambaye aliweza kumuponyesha.
Mutu akiwa na mali ya dunia hii naye akimwona ndugu yake katika hitaji, lakini hataki kumusikilia huruma, mutu yule anaweza kusema kwamba anamupenda Mungu?