Mara moja wakubwa wenzake wakavua nguo zao, wakazilundika pamoja kwenye ngazi kusudi asimame juu yake, wakapiga baragumu na kulalamika kwa sauti: “Yehu ni mufalme!”
Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.