akiwaambia: “Mwende katika kijiji kinachokuwa mbele yenu. Wakati mutakapofika kule, mutaona mwana-punda amefungwa, na hakuna mutu aliyekwisha kupanda juu yake. Mumufungue na kumuleta hapa.
Yeye hahitaji kushugulikiwa na watu, kama vile angekuwa na lazima ya musaada fulani. Kwa maana yeye ndiye anayewapa watu wote pumzi ya uzima, pamoja na vitu vyote wanavyohitaji.
Kwa maana munajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, ingawa alikuwa tajiri, yeye mwenyewe alijifanya masikini kwa ajili yenu, kusudi mupate kuwa watajiri kwa njia ya umasikini wake.