Katika maono mengine, Yawe alinionyesha Kuhani Mukubwa Yoshua akisimama mbele ya malaika wa Yawe, na kwa upande wake wa kuume Shetani alisimama kwa kumushitaki.
“Munapoomba, musikuwe kama wanafiki, kwa maana wanapenda kuomba wakisimama katika nyumba za kuabudia na pembeni ya barabara, kusudi wapate kujionyesha mbele ya watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.
Yule Mufarisayo akajitenga na mwenzake akiomba hivi: ‘Ee Mungu, ninakushukuru kwa sababu mimi si kama watu wote wengine wanaokuwa wanyanganyi, watenda maovu, wazinzi. Ninakushukuru vilevile kwa kuwa mimi si kama huyu mulipishaji wa kodi.
Lakini yule mulipishaji wa kodi alisimama kwa mbali, naye hakusubutu hata kuinua macho yake kuelekea mbingu; lakini alijipigapiga kwa huzuni na kusema: ‘Ee Mungu, unisamehe mimi mutenda mabaya.’ ”
“Musiwahukumu wengine, na Mungu hatawahukumu ninyi. Musikuwe wenye kukatia wengine azabu, naye hatawaazibu ninyi. Muwasamehe wengine, na Mungu atawasamehe ninyi vilevile.
Muvumiliane na kusameheana ninyi kwa ninyi wakati wowote mutu anapokuwa na neno la kumushitaki mwingine. Munapaswa kusameheana kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi.