Kisha wakafika Yerusalema. Yesu alipoingia ndani ya hekalu, akaanza kufukuza watu waliokuwa wakiuzishia na kununulia vitu vyao ndani ya hekalu. Akapindua meza za wale waliobadilisha feza na viti vya wachuuzi wa njiwa.
Kisha akawafundisha maneno haya: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya maombi kwa mataifa yote.’ Lakini ninyi mumeigeuza kuwa nafasi ya kukutania ya wanyanganyi!”